Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Je wajua magunzi ya msonobari ni lulu iliyofichika?

Je wajua magunzi ya msonobari ni lulu iliyofichika?

Pakua
Mbegu za misonobori ni maarufu sana kwenye mapishi, lakini magunzi yake hugeuka adha kwa mazingira. Nchini Tunisia mhitimu wa Chuo Kikuu baada ya kukosa ajira alipata wazo la kutumia taka hizo kuzalisha mboji ambayo sio tu inamwongezea kipato bali pia inalinda mazingira kwa kuondoa taka na pia kuepusha wakulima kutegemea mbolea za viwandani pekee ambazo huchafua vyanzo vya maji ardhini. Wazo lake lilipata msukumo wa kiufadhili kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD na serikali ya Tunisia na tangu aanze biashara hiyo mwezi Januari mwaka huu ameshauza tani 40 na soko linazidi kupanuka. Je ni nini hasa kinafanyika? Fuatana na Assumpta Massoi kwenye makala hii.


 

Audio Credit
Flora Nducha/Assumpta Massoi
Sauti
3'59"
Photo Credit
IFAD