Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR: Utoaji wa vitambulisho kwa wakimbizi nchini Ethiopia waboresha maisha yao

UNHCR: Utoaji wa vitambulisho kwa wakimbizi nchini Ethiopia waboresha maisha yao

Pakua

Wakati dunia hapo jana Juni 20 ikiwa imeadhimisha siku ya wakimbizi duniani na wito kutolewa kila kona wa kuhakikisha wakimbizi wanajumuishwa katika masuala yote ya kuweza kuwasaidia kustawi katika nchi wanayopatiwa hifadhi hii leo tunaelekea nchini Ethiopia kujionea namna mradi wa kutoa vitambulisho vya kitaifa ambao unajumuisha wakimbizi na wasaka hifadhi ulivyobadiliasha maisha ya wakimbizi. 

Makala hii iliyoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR inathibitisha namna mradi huo wa vitambulisho vya kitaifa uliofadhiliwa na Benki ya Dunia umeleta matumaini pamoja na upatikanaji wa ajira kwa wakimbizi na hivyo kuwaondoa katika kundi la watu tegemezi kwani sasa wanaweza kufanya shughuli za kuwaingizia kipato. Leah Mushi anatujuza zaidi. 

Audio Credit
Assumpta Massoi/Leah Mushi
Sauti
3'8"
Photo Credit
UNHCR