Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Watu wakichota maji ya kunywa huko Rafah kusini mwa Gaza
© UNRWA

Gaza: Huko Raha hofu yatanda, wagonjwa wahofia kusaka huduma

Hofu kubwa ikiendelea kutanda huko Rafah, kusini mwa Gaza wakati huu ikiripotiwa kuwa Israel inataka kuelekeza operesheni zake za kijeshi kwenye eneo hilo, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni ,WHO linasema hospitali tayari zimezidiwa uwezo kwani Umoja wa Mataifa umekuwa unasema operesheni hiyo ya kijeshi itasababisha idadi kubwa ya vifo na majeruhi ambao watahitaji huduma za afya.

Kaskazini mwa Gaza iko kwenye magofu baada ya miezi kadhaa ya mashambulizi ya mabomu.
© WFP/Ali Jadallah

Wananchi wa Gaza wako katika jakamoyo wakisubiri taarifa kuhusu wito wa kusitisha mapigano: UN

Wakati kukiwa na ongezeko la wito wa kimataifa kwa Israel kujizuia na mashambulizi zaidi Gaza na ripoti za leo za mashambulizi mengine mabaya zaidi ya usiku kucha, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesisitiza kuhusu athari mbaya zinazoendelea za vita hiyo na haja ya kuhakikisha njia za kuaminika za usambazaji wa misaada kwa watu wanaohitaji kwa udi na uvumba zinapatikana. 

Sauti
1'57"