Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Olle Mjengwa mshiriki wa Jukwaa la Vijana 2030, la Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa, ECOSOC, akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kandoni mwa mkutano huo uliofanyika kwa siku tatu, New York ,Marekani.
UN/Assumpta Massoi

UNDP yashindanisha vijana kusaka majawabu kwa tabianchi , washindi kupata kitita cha fedha

Vijana wameelezwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kusongesha mbele moja ya ajenda kubwa za 2030 za Umoja wa Mataifa ambayo ni kukabiliana na janga la mabadiliko ya tabianchi. Na katika kutambua mchango wao Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP, limekuja na mbinu mbalimbali za kuwashirikisha vijana ili wasiachwe nyuma katika suala hilo na mengine kama ya kuleta amani na usalama. Olle Mjengwa anayefanyakazi ya UNDP ofisi ya Roma Italia amezungumza na UN News kandoni mwa Jukwaa la vijana la Baraza la Kiuchumi na Kijamii ECOSOC lililokunja jamvi mwishoni mwa wiki ili kufafanua kuhusu ushirikishwaji huo wa vijana katika UNDP

 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa na washiriki wengine wa tukio la Kwibuka30 wakiwasha mishumaa kukumbuka waliopoteza maisha wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda yaliyofanyika kwa siku 100 kuanzia Aprili 7, 1994
UN /Eskinder Debebe

Kwibuka30: Vijana kemeeni kauli za chuki kokote muisikiapo na muionapo – Guterres

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Baraza Kuu limekuwa na tukio maalum la kumbukizi ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda au KWIBUKA30, ambapo Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametumia hotuba yake pamoja na mambo mengine kuwasihi vijana kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kukemea chuki kokote wanapoisikia au kuiona.