Wasiwasi mkubwa watanda Gaza kutokana na hofu ya mashambulizi Rafah: UN
Raia wa kawaida wa Gaza bado wako katika hali ya kiwewe kutokana na shambulio kamili la Israel linalokaribia kufanywa kwenye mji wa kusini wa Rafah, huku kukiwa na ongezeko la mashambulizi huko, amesema mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA.