Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Watu wakiwa wamekusanyika nje ya Hospitali ya Al Shifa Gaza ambako kumepatikana makaburi ya halaiki
WHO

GAZA: Makaburi ya halaiki yaonesha waathirika walikuwa wamefungwa mikono - OHCHR

Ripoti za kutisha zinaendelea kuibuka kuhusu makaburi ya halaiki huko Gaza ambako waathirika wa Kipalestina wameripotiwa kuvuliwa nguo wakiwa wamefungwa mikono, jambo ambalo limezusha wasiwasi juu ya uwezekano wa  kuweko kwa vitendo vya uhalifu wa kivita huku kukiwa na mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR.

Baraza Kuu lilipitisha azimio mwaka 2012 lililoipa Palestina hadhi ya kuwa nchi isiyokuwa mwanachama katika Umoja wa Mataifa. (faili)
UN Photo/Rick Bajornas

Hadhi ya Palestina ndani ya UN yafafanuliwa 

Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.

Katibu Mkuu António Guterres akihutubia mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu hali ya Mashariki ya Kati, likiwemo swali la Wapalestina.
UN Photo/Manuel Elías

Guterres ahimiza mashariki ya Kati kujizuia zaidi

Kuongezeka kwa hivi karibuni kwa mzozo huko Mashariki ya Kati kunafanya kuunga mkono juhudi za amani ya kudumu kati ya Israel na taifa huru kabisa la Palestina linaloweza kuwepo na linalojitawala kikamilifu kuwa muhimu zaidi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo.