Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Hukumu ikisomwa wakati wa kesi dhidi ya Ayyash na wenzake baada ya kupatiakana na hatia ya mauaji kwenye shambulio la mwaka 2005 huko Beirut, Lebanon. (Maktaba)
Mahakama Maalum kwa Lebanon

Lebanon: Haki imetendeka, Mahakama Maalum yafunga pazia, Guterres atuma shukrani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amepongeza kazi kubwa na ngumu iliyofanywa na majaji na wafanyakazi wa Mahakama Maalum kwa ajili ya Lebanon, iliyoanzishwa kuwajibisha wahusika wa shambulio la Februari 14 mwaka 2005 huko Beirut. Mahakama hiyo imemaliza muda wake leo Jumapili Desemba 31, baada ya kufanya kazi kwa miaka 14.

Moja ya familia iliyotawanywa kutoka Al Ganoub Oktoba 2023.
OCHA/Manal Massalha

Watoto waliouawa Ukingo wa Magharibi na Jerusalem Mashariki, idadi haijawahi kushuhudiwa

Mwaka huu umekuwa mwaka mbaya zaidi kuwahi kurekodiwa kwa watoto katika Ukingo wa Magharibi, ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki, huku ghasia zinazohusiana na migogoro zikifikia kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa, amesema Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kanda ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Adele Khodr.  


 

Mwonekano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wanachama wanapiga kura kuunga mkono rasimu ya azimio kuhusu hali ya Mashariki ya Kati tarehe 22 Desemba 2023.
UN Photo/Loey Felipe

Kura za Baraza la Usalama zapitisha Azimio zito kuhusu Gaza

Mchana huu wa Ijumaa 22 Novemba saa za New York, Marekani, Baraza la Usalama limeidhinisha azimio linalozitaka pande zinazohusika katika mzozo wa Gaza kuruhusu usambazaji wa haraka wa msaada wa kibinadamu kwa raia wa Palestina katika Ukanda wote wa Gaza. Nyaraka hiyo pia inataka hatua za haraka zichukuliwe ili kuunda mazingira ambayo yanasababisha usitishaji endelevu wa uhasama. Maandishi hayo yameidhinishwa kwa kura 13 za ndiyo, huku Marekani na Urusi zikijiepusha kupiga kura.