UN na wadau wazindua ombi la dola bilioni 2.8 kwa ajili ya Gaza na Ukingo wa Magharibi
Umoja wa Mataifa na mashirika wadau leo wamesisitiza kwamba "mabadiliko muhimu yanahitajika ili kuboresha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu huko Gaza, wakati walizindua ombi la dola bilioni 2.8 kutoa msaada wa dharura kwa watu zaidi ya milioni 3 katika eneo hilo lililoharibiwa, lakini pia katika Ukingo wa Magharibi, ambapo Wapalestina wamekuwa wakilengwa na kuongezeka kwa vurugu za walowezi wa Kiyahudi”.