Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Gari lililosheheni mali na vifaa vya nyumbani linapita kwenye mitaa ya Khan Younis.
© UNOCHA/Themba Linden

UN na wadau wazindua ombi la dola bilioni 2.8 kwa ajili ya Gaza na Ukingo wa Magharibi

Umoja wa Mataifa na mashirika wadau leo wamesisitiza kwamba "mabadiliko muhimu yanahitajika ili kuboresha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu huko Gaza, wakati walizindua ombi la dola bilioni 2.8 kutoa msaada wa dharura kwa watu zaidi ya milioni 3 katika eneo hilo lililoharibiwa, lakini pia katika Ukingo wa Magharibi, ambapo Wapalestina wamekuwa wakilengwa na kuongezeka kwa vurugu za walowezi wa Kiyahudi”.

Watoto wanatibiwa katika hospitali ya muda huko Mouraj, kitongoji kilichoko kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© WHO/Christopher Black

UN WOMEN: Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza

Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza tangu kuzuka kwa vita miezi sita iliyopita na mtoto mmoja anajeruhiwa au kufariki dunia kila baada ya dakika 10, yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo huku kukiwa na ongezeko la ghasia katika Ukingo wa Magharibi na wasiwasi wa kuongezeka kwa mzozo wa kikanda kufuatia makombora ya Iran kushambulia Israeli.

Gari linaendeshwa kupitia vifusi huko Khan Younis.
© UNOCHA/Themba Linden

Wataalamu wa haki za binadamu wanalaani jukumu la AI kwa uharibifu unaofanywa na jeshi la Israel Gaza

Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akirejelea ombi lake la hali ya kujizuia kwa kiwango cha juu zaidi Mashariki ya Kati kufuatia shambulio la ndege zisizo na rubani na kombora la Iran dhidi ya Israeli, wataalam huru wa haki za binadamu wamesema madai ya utumiaji wa kijasusi wa akili mbemba au bandia kwenye maeneo ya Gaza unaofanywa na jeshi la Israeli umesababisha athari zisizo na kifani kwa raia, nyumba na huduma.

Watoto waliokimbia makazi yao wanatafuta chakula karibu na mahema wanamoishi na familia zao, katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza...
© UNICEF/Eyad El Baba

GAZA: Gari la UNICEF lashambuliwa, watoto taabani kwa kula nyasi

Huko ukanda wa Gaza ambako ni nusu mwaka sasa tangu mashambulizi yaanze baada ya wapiganaji wa Hamas kushambulia Israel Oktoba 7, 2024, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, limetangaza kwamba moja ya magari yake lilishambuliwa kwa risasa za moto jana Jumatano wakati likisubiri kuingia kaskazini mwa Gaza kutokea kusini mwa eneo hilo.

Uopoaji wa miili kutoka chini ya vifusi vya nyumba katika kitongoji cha Al-Nasr, mashariki mwa mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
UN News/Ziad Taleb

Baraza la Usalama kujadili ombi la Palestina kuwa mwanachama wa UN

Huko Gaza, watoa misaada ya kibinadamu wakiwa na wasiwasi mkubwa juu ya mipango ya Israel kuvamia eneo la Rafah hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa Palestina imeanza mchakato wa kuwa mwanachama rasmi wa Umoja wa Mataifa kwani hivi sasa ujumbe wake ni uangalizi usioipatia hadhi ya kupiga kura. Mchakato huo unaanzia ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. 

Sauti
2'24"