Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto katika kambi za wakimbizi wa ndani nchini Afghanistan
© UNICEF/Omid Fazel

Tuendeleze mazungumzo na wataliban Afghanistan: Mwakilishi wa UN

Licha ya misimamo tofauti kati ya serikali inayoongozwa na wataliban nchini Afghanistan, na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini humo, UNAMA, lazima tuendelee na mazungumzo kwa maslahi ya wananchi wa taifa hilo la Asia, amesema Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan, UNAMA wakati akihutubia Baraza la Usalama Jumanne ya tarehe 20 Desemba 2022.

Wasichana wadogo wakiwa nyumbani kwao huko grand Turk, ambayo iliharibiwa vibaya wakati kimbunga Irma kilipopiga Visiwa vya Turks na Caicos.
© UNICEF/Manuel Moreno Gonzalez

Mashirika ya UN kuunda mfumo wa kukabiliana na majanga

Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Mpango wa maendeleo duniani, UNDP, Hali ya hewa Duniani WMO pamoja na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya upunguzaji hatari za majanga UNDRR yanashirikiana kutengeneza mfumo mpya wa ufuatiliaji, kurekodi na kuchambua majanga hatari pamoja na hasara na uharibifu unaosababishwa na matukio hayo.

Oscar Kalere Oscar, mhamiaji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na anaaishi nchini Tanzania tangu mwaka 2002 na sasa anafanya kazi ya uchungaji.
UN News

Asante Umoja wa Mataifa kupitia uhamiaji sasa nina familia Tanzania- Oscar

Ikiwa ni siku chache zimepita tangu dunia kuadhimisha siku ya wahamiaji duniani, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la uhamiaji, IOM,  ukitoa wito kwa jamii ya kimataifa na nchi wanachama wa Umoja huo  kushiriki katika kufanikisha uhamiaji wa wale wanaokimbia ghasia makwao na halikadhalika wale wanaosaka fursa bora, mmoja wa wanufaika wa uhamiaji ametoa shukrani zake kwa taifa ambalo limempatia hifadhi baada ya kukimbia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Mwanamke asiye na makazi akiomba pesa katika nji wa London, Uingereza
Unsplash/Tom Parsons

Wataalamu wa UN wanalaani mashambulizi dhidi ya waathirika wa utumwa wa kisasa na usafirishaji haramu wa binadamu nchini Uingereza

Kuwaandama waathirika wa usafrishaji haramu wa binadamu na aina za utumwa za kisasa kunaondoa huruma ya umma katika hatua za kuwalinda na huenda ikasababisha mashambulizi ya watu wenye itikadi kali dhidi ya makundi hayo, wataalam wa Umoja wa Mataifa wameonya leo, wakiitaka Uingereza kuongeza juhudi za kuwalinda manusura. 

CBD umepitisha makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika mkutano huo kuhusu mpango mpya wa kuhifadhi na kulinda asili kwa kutumia Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai, (GBF).
Picha: UN Biodiversity

Jumuiya ya kimataifa na wadau wa mazingira wakaribisha Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai (GBF)

Ikiwa leo ni tamati ya mkutano wa 15 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa kuhusu bayonuai, COP15, huko Montréal, Canada, wadau mbalimbali wa mazingira wamekaribisha makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa katika mkutano huo kuhusu mpango mpya wa kuhifadhi na kulinda asili kwa kutumia Mfumo mpya wa Kimataifa wa Bayonuai, (GBF).

Sauti
1'54"