Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Nyiranzaba na watoto wake tisa wanapata hifadhi kwenye hema baada ya kukimbia kijiji chake katika eneo la Rutshuru, jimbo la Kivu Kaskazini, DR Congo.
© UNICEF/Arlette Bashizi

Vurugu za sasa DRC ni ishara ya onyo - Mshauri Maalumu wa UN kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari 

Kufuatia ziara yake rasmi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuanzia tarehe 10-13 Novemba 2022, Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari, Alice Wairimu Nderitu amesikitishwa sana na kuongezeka kwa ghasia katika Ukanda wa Maziwa Makuu ambako Mauaji ya Kimbari yam waka 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda yalitokea.