Vurugu za sasa DRC ni ishara ya onyo - Mshauri Maalumu wa UN kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari
Kufuatia ziara yake rasmi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuanzia tarehe 10-13 Novemba 2022, Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari, Alice Wairimu Nderitu amesikitishwa sana na kuongezeka kwa ghasia katika Ukanda wa Maziwa Makuu ambako Mauaji ya Kimbari yam waka 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda yalitokea.