Nchi tatu zaidi Afrika zagundua kuwa na wagonjwa wa Monkeypox
Wakati nchi tatu ambazo awali hazikuwa na historia ya kuwa na ugonjwa wa ndui ya nyani au Monkeypox zikiripoti kuwa na wagonjwa katika mataifa yao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika imetangaza kuanza kufanya kazi na mataifa ya Afrika katika kuimarisha uwezo wa nchi kufanya uchunguzi wa kimaabara ili kubaini wagonjwa hao kwa haraka na kuzuia kuenea kimya kimya kwa ugonjwa huo.