Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Picha iliyokuzwa sana inaonesha chembe ya virusi aina ya mulberry kirusi cha Monkeypox ambayo ilipatikana kwenye umajimaji wa malengelenge ya binadamu.
© CDC

Nchi tatu zaidi Afrika zagundua kuwa na wagonjwa wa Monkeypox

Wakati nchi tatu ambazo awali hazikuwa na historia ya kuwa na ugonjwa wa ndui ya nyani au Monkeypox zikiripoti kuwa na wagonjwa katika mataifa yao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika imetangaza kuanza kufanya kazi na mataifa ya Afrika katika kuimarisha uwezo wa nchi kufanya uchunguzi wa kimaabara ili kubaini wagonjwa hao kwa haraka na kuzuia kuenea kimya kimya kwa ugonjwa huo.

Rekodi ya watu milioni 11.7, karibu robo ya wakazi wa Sudan, wanatarajiwa kukabiliwa na njaa katika kilele cha msimu wa mwambo mwezi Septemba.
©FAO/Ahmedalidreesy Adil

WHO yaanzisha kituo maalum cha kusaidia wananchi wa Pembe ya Afrika

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO limetangaza kuongeza shughuli zake katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuanzisha kituo maalum cha huduma jijini Nairobi nchini Kenya wakati huu eneo hilo likikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula unaosababishwa na migogoro, matukio mabaya ya mabadiliko ya tabianchi ikiwa ni pamoja na ukame mbaya zaidi kushuhudiwa katiak kipindi cha miaka 40, kupanda kwa bei ya chakula kimataifa pamoja na bei ya mafuta.

 Bandari ya uvuvi ya Joal nchini Senegal.
© FAO/Sylvain Cherkaoui

Shughuli za uvuvi na ufugaji wa Samaki zinatoa mchango mkubwa kwenye uhakika wa upatikanaji wa chakula :FAO

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari ukiwa katika siku ya tatu hii leo huko Lisbon nchini Ureno Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ongezeko kubwa la ufugaji wa samaki sambamba na uvuvi wa kimataifa umesababisha mazao ya vyakula vya majini kuwa kwenye rekodi ya juu katika kuchangia kwa kiasi uhakika wa chakula na lishe katika karne hii ya Ishirini na moja.

Sauti
2'26"
Watoto wa kike wanakuwa hatarini kuozeshwa mapema na wengi wao ni wale wanaotoka familia maskini na makundi ya pembezoni
©UNFPA-UNICEF Nepal/KPanday

Ndoa za utotoni zashamiri Pembe ya Afrika - UNICEF

Watoto wa kike wenye umri mdogo hata miaka 12 huko Pembe ya Afrika wanalazimishwa kuolewa sambamba na kukeketwa au FGM, katika viwango vya kutisha wakati huu ambapo ukame mkali kuwahi kukumba eneo hilo katika kipindi cha miaka 40 ukisukuma familia katika mazingira magumu, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF.

Amiri Juma Amiri mkulima huyu wa mwani akiwa na mwani aliovuna kutoka shambani kwake baharini kufuatia mradi unaofadhiliwa na taasisi ya utafiti wa majini na viumbe vya  bahari ya Kenya.
UN/ Kenya

Kilimo cha mwani baharini kimenitoa kwenye nyumba ya tope – Amiri wa Kibuyuni, Kwale - Kenya

Moja ya malengo ya Mkutano wa bahari unaoendelea Lisbon, Ureno, ni kujadili namna ambavyo dunia inaweza kuendelea kunufaika kiuchumi kutokana na uwepo wa bahari. Ajenda hiyo inakuwa muhimu kwa kuwa tayari ni dhahiri baharí imekuwa mkombozi wa kiuchumi kwa watu wengi duniani. Mfano wa wazi ni Amiri Juma Amiri, mkazi wa kijiji cha Kibuyuni katika Kaunti ya Kwale huko Pwani ya Kenya, mkulima wa zao la mwani ambalo hulimwa baharini.

Sauti
2'58"