Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Askari wa kulinda amani wakisindikiza msafara wa misaada ya kibinadamu kuelekea kijiji cha Pinga huko Kivu Kaskazini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Guy Hubbard

Baraza la Usalama ungeni mkono kwa dhati hatua za kutokomeza M23- Bi. Pobee 

Ongezeko la hivi karibuni la mashambulizi kutoka kikundi cha waasi cha M23 huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linatishia amani, usalama na  utulivu kwenye ukanda mzima wa Maziwa Makuu barani Afrika na hivyo hatua za dharura za kudhibiti ghasia hizo zinahitajika, amesema Afisa Mwandamizi wa Umoja wa Mataifa hii leo wakati akihutubia Baraza la Usalama la umoja huo jijini New York, Marekani. 

Majanga ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa inasababisha watu kukimbiz makwao.
© UNFPA Ethiopia/Paula Seijo

Zaidi ya watu milioni 30 walifungasha virago 2020 kutokana na majanga:UNDRR

Zaidi ya watu milioni 30 walikimbia makazi yao kutokana na majanga mwaka 2020 pekee, na idadi hii huenda ikaongezeka kutokana na kuongezeka kwa hatari na idadi ya matukio makubwa yanayohusiana na hali ya hewa. Jopo katika Kikao cha 7 cha Jukwaa la Kimataifa la Kupunguza Hatari za majanga (GPDR2022), lililosimamiwa na Sarah Charles, Msimamizi Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani, limeangazia mbinu za kuimarisha utawala ili kupunguza hatari za majanga ya kuhamishwa.

Wanawake kutoka nchini Sudan wakitembea mahali salama Um Baru, Kaskazini mwa Darfur.
UNAMID/Hamid Abdulsalam

FAO yatoa dola milioni 12 kusaidia wananchi wa Sudan

Juhudi zinazofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO za kusaka misaada kwa ajili ya wananchi wa Sudan wanaokabiliwa na njaa, ukame, na hali ngumu ya maisha ambayo kwa ujumla imechochewa na vita ya Ukraine zimezaa matunda baada ya mradi wao mpya kupata ufadhili wa dola milioni 12 kutoka Mfuko wa kukabiliana na dharura wa Umoja wa Mataifa CERF.

Wanaharakazi vijana wakishiriki mgomo kwa ajili ya kuchagiza kuhusu mabadiliko ya tabianchi Stockholm, Sweden.
© UNICEF/Christian Åslund

Hatua zichukuliwe sasa kulinda mazingira la sivyo binadamu watageuka kafara: wataalam UN 

Miongo mitano baada ya kongamano la kwanza la dunia la kufanya mazingira kuwa suala kuu, wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wametoa wito kwa mataifa kuongeza juhudi za kulinda sayari iliyo hatarini kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo huku kukiwa na changamoto ambazo hazijawahi kushuhudiwa za mazingira na nyinginezo.