Watu nusu milioni wakimbia nyumba zao Ukraine, 330,000 waingia nchi jirani:UN
Huku mashambulizi ya Urusi yakiendelea katika miji ya Ukraine, takriban raia nusu milioni wamekimbia makazi yao, na theluthi mbili kati yao wamevuka mipaka ya kimataifa kutafuta hifadhi katika nchi jirani, Umoja wa Mataifa umesema leo Jumapili Februari 27 .