Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Soko nchini Sudan Kusini
© UNICEF/Sebastian Rich

UNMISS yapatia mafunzo wafanyabiashara Sudan Kusini ili wafanye biashara kwa ufanisi

Ushirikiano na ukuaji kiuchumi ni miongoni mwa masuala muhimu katika kuhakikisha nchi yoyote ina amani na wananchi wake wanapata Maendeleo. Na ili kuhakikisha wananchi wa Sudan Kusini wana amani na maendeleo, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda Amani nchini humo UNMISS umeandaa warsha ya biashara lengo likiwa ni kuwatia moyo wafanyabiashara wa ndani na kuwawezesha kiuchumi ili nao waweze kuimarisha biashara zao lakini pia waweze kufanya biashara na Umoja wa Mataifa .

Sauti
3'34"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Morocco ambao walijeruhiwa wakati wa makabiliano kati ya jeshi la serikali la DRC, FARDC na waasi wa M23 huko Kiwanja, Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini wakisafirishwa kwa matibabu zaidi.
MONUSCO

Umoja wa Mataifa wasikitishwa sana na kuibuka tena kwa mapigano DRC

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesikitishwa sana na kuibuka tena kwa mapigano tangu tarehe 20 Oktoba,2022 kati ya vikosi vya jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, FARDC na kundi la wapiganaji waasi la M23 ambayo yamesababisha vifo vya raia, kusababisha watu kuyakimbia makazi yao na kujeruhiwa kwa walinda amani wanne wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO.

Meli ya kwanza ya kibiashara ikiwa na nafaka kupitia mpango wa usafirishaji wa nafaka kupitia Bahari Nyeusi
© UNOCHA/Levent Kulu

UN yaingiwa hofu kufuatia Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka Bahari Nyeusi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya uamuzi wa Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka kupitia Bahari Nyeusi, au kwa kiingereza, Black Sea Grain Initiative, makubaliano ambayo yalianzishwa tarehe 22 mwezi Julai mwaka huu ili kuwezesha Ukraine kuanza kuuza tena nje ya nchi hiyo vyakula na mbolea.

Nchini Niger kama maeneo mengine mengi ya Sahel, madhara ya mabadiliko ya tabianchi yamezidisha vipindi vya ukame na hivyo watu kuhama makazi yao na kusaka maeneo mengine huku wakitegemea zaidi  misaada
© FAO/IFAD/WFP/Luis Tato

Mabadiliko ya tabianchi yanazidi kuongeza idadi ya wakimbizi wa ndani:UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi UNHCR, limetahadharisha ongezeko la wakinbizi  huko Sahel na kutoa ombi la msaada wa haraka wa mahitaji ya kibinadamu kwa zaidi ya watu milioni 3.4 waliokimbia makazi yao na wenyeji wao kutokana na mafuriko makubwa yaliyozikumba nchi za Nigeria, Chad, Niger, Burkina Faso, Mali na Cameroon hivi karibuni. 

Moishe Holzberg akiwa na Mama mlezi wake Sandra Samuel ambaye kwa ujasiri mkubwa alimwokoa wakati wa shambulio la kigaidi Tah Mahal Palace Hotel mwaka 2008 nchini India. Wakati huo Moishi alikuwa na umri wa miaka miwili.
Picha kwa hisani ya Moishe Holzberg

Manusura wa ugaidi waitaka UN ihakikishe hakuna eneo linakuwa rafiki kwa ugaidi

“Ombi langu kwa wawakilishi wote wa nchi wahakikishe hakuna eneo lolote linakuwa salama kwa ugaidi,” amesema Nidhi Chaphekar, manusura wa shambulio la kigaidi la mwaka huko Brussels nchini Ubelgiji. Kauli  yake hiyo ameitoa huko India hii leo Ijumaa wakati wa ufunguzi wa mkutano maalum wa Kamati ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na ugaidi.

Mji mkuu wa Nairobi, Kenya
World Bank/Sambrian Mbaabu

Heko Kenya kwa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa- UN

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017

Sauti
1'59"