Jukwaa laanzishwa mtandaoni kuongeza ufahamu wa uhusiano kati ya tabianchi na afya
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la afya ulimwenguni, WHO na la hali ya hewa, WMO leo yamezindua jukwaa maalum la kuongeza ufahamu juu ya uhusiano kati ya tabianchi na afya, likiwa ni jukwaa la kwanza kabisa la aina yake.