UNSMIL ya Libya yaongezewa miezi mitatu zaidi
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo kwa kauli moja limepitisha azimio la kuongeza muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini Libya, UNSMIL hadi tarehe 30 mwezi huu wa Aprili.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo kwa kauli moja limepitisha azimio la kuongeza muda wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini Libya, UNSMIL hadi tarehe 30 mwezi huu wa Aprili.
Kufuatia majuma kadhaa ya mvutano mkali nchini Ukraine, na ripoti kwamba Urusi imekuwa ikipeleka zaidi ya wanajeshi 100,000 na silaha nzito karibu na mpaka wake, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo limefanya mkutano wake wa kwanza kujadili njia za kupunguza mzozo huo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na UKIMWI, UNAIDS limeeleza kuwa katika maambukizi mengi mapya 150,000 ya Virusi Vya UKIMWI miongoni mwa wa watoto katika mwaka 2020, yangeweza kuzuiwa.
Raia 272 kutoka familia 78 wa Burundi waliorejea nchini Burundi kutoka kambi ya wakimbizi ya Lusenda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa wiki iliyopita wamekaribishwa na wanachi wenzao, serikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ili waanze maisha katika nchi yao waliyoikimbia kwa vipindi tofauti kutokana na hali mbaya ya usalama
Mfuko wa Elsie wa kufadhili wanawake walioko kwenye operesheni za ulinzi wa amani, EIF, hii leo umetangaza mchango wa dola 357,000 kwa ajili ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Lebanon, UNFIL.
Wataalamu wa kimataifa wa mawasiliano ya redio kwa kushirikiana na nchi za Afrika hii leo wametambulisha masafa mapya kati ya 87.5 megahertz (MHz) na 108 MHz ili kupanua huduma za utangazaji za redio za FM ikiwa ni urekebishaji wa masafa katika bara zima.
Ikiwa hapo kesho Jumanne, Februari 1,2022 ni maadhimisho ya mwaka mmoja tangu jeshi la Myanmar kupindua Serikali ya kiraia iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia na kuwaweka kizuizini kiholela viongozi wa Serikali, akiwemo Mshauri wa Serikali Aung San Suu Kyi na Rais Win Myint. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema anasimama katika mshikamano na watu wa Myanmar na matarajio yao ya kidemokrasia kwa jamii jumuishi na ulinzi wa jamii zote, ikiwa ni pamoja na Rohingya.
Katika maadhimisho ya Siku ya Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele Duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa wito kwa kila mtu, kujiunga pamoja ili kukabiliana na ukosefu wa usawa unaojitokeza katika magonjwa yasiyo ya kuambukiza na kuhakikisha jamii maskini zaidi na zilizotengwa ambazo zimeathiriwa zaidi na magonjwa ya kitropiki yaliyosahaulika zinapata huduma za afya wanazohitaji.
Leo ni siku ya Ukoma duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka 2022 ni Umoja kwa Utu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewatumia ujumbe wa heri ya mwaka mpya wakichina wananchi wa China ambao wanasherekea mwaka wa Simba Marara