Tusipoipa kisogo tunaweza kuinusuru Afghanistan na mahitaji yake ya kibinadamu:UN
Wakati dunia inaelekeza nguvu zake katika vita vinavyoendelea nchini Ukraine, Umoja wa Mataifa hii leo umeikumbusha jumuiya ya kimataifa kuikumbuka Afghanistan wakati ukizindua mkutano wa ahadi za msaada wa kuokoa maisha ya mamilioni ya watu wa taifa hilo lisilo na bandari.