Watoto nchi nzima ya Afghanistan wapatiwa chanjo za Surua na Polio
Zaidi ya watoto milioni 5 nchini Afghanistan wenye umri wa kuanzia miezi 9 hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya surua ilhali watoto zaidi ya milioni 6 wenye umri wa kuanzia kuzaliwa hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya polio katika kampeni ya kitaifa iliyoanza mwezi uliopita wa Novemba hadi tarehe 12 mwezi huu wa Desemba.