Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Msichana mdogo akipokea chanjo yake ya surua na polio kama sehemu ya kampeni ya chanjo ya nchi nzima nchini Afghanistan.
© WHO Afghanistan

Watoto nchi nzima ya Afghanistan wapatiwa chanjo za Surua na Polio

Zaidi ya watoto milioni 5 nchini Afghanistan wenye umri wa kuanzia miezi 9 hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya surua ilhali watoto zaidi ya milioni 6 wenye umri wa kuanzia kuzaliwa hadi miaka 5 wamepatiwa chanjo dhidi ya polio katika kampeni ya kitaifa iliyoanza mwezi uliopita wa Novemba hadi tarehe 12 mwezi huu wa Desemba.

Mafuriko ya hivi karibuni nchini Sudan Kusini
Picha: UN News

Msaada wa dola milioni 14 kutoka CERF kunufaisha zaidi ya watu 260,000 Sudan Kusini

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya dharura, Martin Griffiths ametangaza kutoa dola million 14 kutoka mfuko mkuu wa dharura wa Umoja huo, CERF kwa ajili ya kupatia misaada ya kibinadamu wananchi wa Sudan Kusini walioathiriwa na ongezeko la mapigano na mafuriko, kwa kuzingatia kuwa ombi la usaidizi kwa taifa hilo bado uchangiaji wake unasuasua. 

Watoto waliokimbia makazi yao kufuatia machafuko. Wanaishi katika kambi ya wakimbizi mipakani ya kusini magharibi mwa Syria.
© UNICEF/Alaa Al-Faqir

Mwaka mpya ukijongea, wito watolewa kuwapa matumaini watu wa Syria

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya kikao cha Baraza la Usalama leo Jumatano, kuhusu hali ya Syria, ambapo limesikiliza taarifa mbili fupi kuhusu hali ya kisiasa na usalama, iliyotolewa  kwa njia ya video na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu kwa Syria Geir Pedersen na Martin Griffiths Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA.

Mwanamke akivuna tumbaku nchini Malawi
© ILO/Marcel Crozet

Watoto watumikishwa kwenye mashamba ya tumbaku Malawi: OHCHR

Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza wasiwasi wao juu ya idadi kubwa ya watoto wanaotumikishwa kwenye mashamba ya tumbaku nchin Malawi, wakitaka serikali na kampuni za tumbaku zinazoendesha shughuli zao nchini humo kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa kwenye mnyororo mzima wa kilimo cha zao hilo.

Wasichana wakiwa darasani katika Kituo cha Kujifunza cha Kasi katika Mkoa wa Wardak katika mkoa wa kati wa Afghanistan.
© UNICEF/Christine Nesbitt

UN yasema wasichana wa Afghanistan kuzuiwa kuhudhuria Chuo Kikuu ni pigo jingine la kikatili kwa haki za wanawake na wasichana

Umoja wa Mataifa umetaka mamlaka za watalibani nchini Afghanistani kubadili uamuzi wake wa kuzuia wasichana kujiunga na elimu ya Vyuo Vikuu nchini humo, tangazo ambalo limetolewa na taifa hilo la barani Asia Jumanne wiki hii ikiwa ni miezi tisa tangu watangaze kuzuia wasichana kuendelea na elimu ya sekondari.

 

Sauti
2'2"