Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mashirika ya UM yajihusisha Kenya kudhibiti mripuko wa kipindupindu Turkana Mashariki

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti Alkhamisi jioni kwamba taasisi kadha za UM zinazohudumia misaada ya kiutu, hivi sasa zinajitahidi kuipatia Serikali ya Kenya misaada ya dharura inayohitajika kupambana na mripuko wa maradhi ya kipindupindu, yaliozuka kwenye eneo la kaskazini-magharibi, ambapo tumearifiwa watu karibu 30 walifariki kutokana na ugonjwa huo, kwenye zile sehemu za mbali zenye matatizo kuzifikia.

Shughuli za Baraza la Usalama kwa Alkhamisi

Mapema asubuhi ya leo, Baraza la Usalama limepitisha azimio la kuongeza muda wa shughuli za Ofisi ya UM juu ya Mchanganisho wa Huduma za Amani Burundi (BINUB) ambazo zinatazamiwa kuendelezwa hadi mwisho wa mwaka 2010.

Hapa na pale

Alkhamisi asubuhi, mataifa 11 yaliripotiwa kuidhinisha na kuridhia Mapatano ya Kimataifa ya 2006 juu ya Mbao za Tropiki (2006 International Tropical Timber Agreement). Nyaraka za Mapatano ziliokusudiwa kukabidhiwa KM, ziliwakilishwa kwenye tafrija iliofanyika katika Ofisi ya UM juu ya Masuala ya Sheria. Mataifa 11 yalioridhia Mapatano ya Mbao za Tropiki ni kama ifuatavyo: Bulgaria; Jamhuri ya Ucheki; Finland; Ujerumani, Ireland; Ureno; Romania; Slovakia; Slovenia na Uspeni. Mapatano ya Mbao za Tropiki, bado hayajakuwa chombo rasmi cha kimataifa na sasa hivi kinajumlisha Makundi Yalioridhia mapatano kutoka nchi arobaini na moja.