UNHCR imetangaza watu 74,000 wa Pembe ya Afrika wamehajiri Yemen 2009 kuomba hifadhi
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti raia 74,000 waliwasili kwenye mwambao wa taifa la Yemen mwaka huu, kutoka eneo la Pembe ya Afrika, watu waliokuwa wakikimbia hali ya mtafaruku uliozuka na kujiepusha mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, pamoja na uegugeu wa kisiasa, hali duni ya maisha, ikichanganyika vile vile na baa la njaa na ukame.