UNAMID imekamilisha thuluthi mbili ya maofisa wa polisi wanaohitajika kulinda raia
Shirika la Vikosi vya Mchanganyiko vya UM-UA kwa Darfur (UNAMID) leo limeripoti kuwasili kwenye mji wa El Fasher, wiki hii, maofisa wa polisi 130 watakaotumiwa kuimarisha usalama kwenye kambi za wahamiaji wa ndani ya nchi.