Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Upigaji marufuku minara ya misikiti Uswiss ni kitendo cha ubaguzi dhidi ya WaIslam, asisitiza mtaalamu wa UM wa haki za binadamu

Asma Jahangir, Mkariri (Mtetezi) Maalumu juu ya uhuru wa kiitikadi na haki ya kufuata dini, ametoa taarifa kwa waandishi habari, kufuatia kura ya maoni iliofanyika Uswiss, ya kupiga marufuku ujenzi wa minara mipya ya misikiti nchini humo, taarifa iliosisitiza kwamba marufuku hayo huwa yanabagua kidhahiri jamii ya WaIslam waliopo katika Uswiss.

Ugonjwa maututi wa sotoka, uliodhuru wakulima miaka iliopita, unakaribia kufyekwa kimataifa

Imetangazwa kutoka Roma, Utaliana, leo hii, yalipo Makao Makuu ya Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) ya kuwa jamii ya kimataifa inakaribia kufyeka milele lile janga maututi la maradhi ya sotoka, ugonjwa wa kuhara wenye kuambukiza ng\'ombe, maradhi ambayo kwa muda wa miaka mingi, yalikuwa yakiwasumbua wakulima, hasa kwenye yale maeneo ya Afrika, kusini ya Sahara.

Hapa na pale

Alkhamisi KM Ban Ki-moon anatazamiwa kusafiri kwenda Trinidad na Tobago kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Serikali Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CHOGM). Kwenye ziara hiyo, itakayochukua siku tatu, KM anatarajiwa kuwahimiza viongozi wa CHOGM kuhudhuria Mkutano Mkuu juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa wa Copenhagen, utakaofanyika mwezi ujao, kikao ambacho kinaandaliwa kujaribu kukamilisha mapatano ya kuanzisha mkataba mpya wa kudhibiti bora athari za mabadiliko ya hali ya hewa. Wakuu wa kiserikali watanasihiwa na KM kuwa na mtazamo halisi utakaowawezesha kufikia mapatano yanayoridhisha kwenye Mkutano Mkuu wa Copenhagen, maafikiano yatakayodumishwa, yenye usawa na yanayotimiza matakwa ya kisayansi.