Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

Kikosi cha pamoja cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika na UM huko Darfur kiliripoti Alhamisi kwamba utulivu wa kiasi fulani umerudi katika eneo lililokua na ghasia la Magharibi ya Sudan, ingawa kungali na wasi wasi juu ya kuendelea ghasia katika baadhi za sehemu. UNAMID inasema kumekua na ripoti za uhalifu huko Darfur ya Kaskazini na wanamgambo wenye silaha wanaendelea kuwashambulia na kuwabughudhi raia huko Darfur ya Kusini

Ripoti ya UM yataka mageuzi katika kikosi cha polisi Kenya

Karibuni wapendwa wasikilizaji katika makala yetu ya ripoti ya wiki leo tutazungumzia ripoti ya mjumbe maalum wa UM kwa ajili ya mauwaji ya kiholela, inayo toa mwito kwa Rais wa Kenya kutambua na kuchukua hatua za kukomesha kile alichokieleza ni "mauwaji yanayopangwa, yaliyoenea na kufanywa kwa ustadi" na polisi wa nchi hiyo.

Hapa na pale

Baraza la usalama limelaani vikali shambulio la kujitoa mhanga dhidi ya kambi ya kikosi cha walinda amani wa Umoja wa afrika AU huko Mogadishu.

Msaada wa dharura wahitajika Somalia

Idara ya kuratibu huduma za dharura za UM, OCHA imeonya kwamba bila ya kuongezwa haraka msaada kukabiliana na janga kubwa la utapia mlo na magonjwa huko Somalia, basi hali hiyo itazidi kuzorota.