Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

Ijumaa asubuhi KM Ban Ki-moon, akijumuika na wafanyakazi wa UM waliopo kwenye Mkao Makuu, pamoja na maofisa wa vyeo vya juu, ikijumlisha Naibu KMAsha-Rose Migiro walikusanyika kwenye Ukumbi wa Baraza la Udhamini kuwakumbuka watumishi wenziwao watano waliouawa Ijumatano, na wapinzani wa Taliban, ndani ya nyumba ya wageni, kwenye mji wa Kabul, Afghanistan. Watumishi waliouawa walitokea Philippines, Marekani, Ghana na Liberia. Mtu wa tano hajatambuliwa bado uraia wake, ikisubiriwa matokeo ya vipimo vya afya vinavyoendelezwa na madakatari kuthibitisha asili ya maiti. Kabla ya wafanyakazi wa UM kusikiliza taarifa ya KM juu ya tukio, na miradi inayoandaliwa kuimarisha usalama wa watumishi wa UM waliopo nje, hasa katika Afghanistan, walisimama wima kimya kwa dakika moja kuwakumbuka na kuwaombea wenziwao waliouawa na shambulio la bomu la kujitoa mhanga. Baadaye mke wa askari wa usalama aliyeuawa kutoka Ghana alihutubia mkusanyiko huo na aliomboleza juu ya kifo cha mumewe, marehemu Lawrence Mefful. Kwenye risala yake, KM alisema UM sasa hivi unafanya mapitio ya dharura juu ya mazingira ya usalama, kwa ujumla, nchini Afghanistan. Alisema UM unazingatia vile vile uwezekano wa kupeleka vikosi ziada vya usalama kuhakikisha majengo ya UM yanapatiwa ulinzi na hifadhi bora kujikinga na mashambulio.

Mkariri wa UM anayetetea haki za wateswa amefukuzwa Zimbabwe

Manfred Nowak, Mtaalamu wa UM juu ya masuala ya mateso, na vitendo vyengine visio vya kiutu vyeye kudhalilisha hadhi ya ubinadamu, alkhamisi alitangaza, kutokea Johannesburg, Afrika Kusini ya kuwa ana wasiwasi juu ya madai ya kuwepo hali mbaya, iliokiuka haki za kiutu za wafungwa, katika magereza ya Zimbabwe, taarifa aliowakilisha saa 24 baada ya kunyimwa ruhusa ya kuingia nchini humo kuendeleza uchunguzi kuhusu madai hayo.