Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na pale

John Holmes, KM juu ya Masuala ya Kiutu na Misaada ya Dharura ameshtumu, kwa kauli kali, mashambulio ya raia yaliofanyika karibuni kwenye jimbo la Kivu Kusini, katika JKK, na kundi la waasi la FDLR.

Baraza la Usalama

Alkhamisi Baraza la Usalama asubuhi lilianza shughuli zake kwa kujadilia hali katika Cyprus, na maendeleo kuhusu mazungumzo ya kusawazisha mfarakano baina ya raia wa Kigiriki na wale wa Kituruki.

Takwimu mpya za WHO juu ya maambukizi ya vimelea vya H1N1

Dktr Keiji Fukuda, Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kwenye mahojiano Alkhamisi na waandishi habari mjini Geneva, alitangaza takwimu mpya juu ya maambukizo ya homa ya mafua ya nguruwe, ambayo kuanzia leo itajulikana rasmi kama homa ya vimelea vya H1N1.

Hapa na pale

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeripoti idadi ya watu walioambukizwa na maradhi ya homa ya mafua ya nguruwe imeongezeka, kwa kulingana na taarifa ilizopokea Ijumatano kutoka maabara ya uchunguzi wa kisayansi wa maradhi.

MONUC imekanusha tetesi za BBC juu ya uhusiano wa CNDP na MONUC

Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika JKK (MONUC) limekanusha kihakika tetesi za ripoti ya shirika la habari la Uingereza la BBC zinazodai John Bosco Ntaganda, mtuhumiwa wa jinai ya vita na kiongozi wa kundi la waasi la CNDP kwenye eneo la kaskazini-mashariki ya JKK, alishiriki kwenye operesheni za vikosi vya UM nchini mwao.

Siku ya kuwakumbuka waathirika wa silaha za kemikali

KM wa UM Ban Ki-moon ameyasihi Mataifa Wanachama kuchukua hadhari kuu ili kuhakikisha silaha maututi za kemikali hazitodhibitiwa katu na makundi ya magaidi. KM aliyasema haya kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kuwakumbuka Waathirika wa Mapigano Yanayotumia Kemikali.