Tume ya Kuchunguza Ukweli juu ya Vita katika Tarafa ya Ghaza, iliobuniwa rasmi mwezi uliopita kwenye kikao maalumu cha Baraza la Haki za Binadamu Geneva, inatarajiwa kuelekea Ghaza mnamo mwisho wa wiki hii, kwa kupitia kivuko cha Rafah, kiliopo upande wa Misri. Tume ya watu watatu, inayoongozwa na Jaji Richard Goldstone wa Afrika Kusini, itawasili Ghaza Juni mosi na itakutana na makundi husika yote na mgogoro wa eneo hilo, ikijumlisha mashirika yasio ya kiserikali, jumuiya za kiraia, mashirika ya UM, waathirika wa mashambulio ya Israel pamoja na kuklutana na wale mashahidi wengine wanaohusika na madai ya kufanyika ukiukaji wa haki za kibinadamu katika eneo liliokaliwa. Tume ya Barazala Haki za Binadamu pia itakutana na watu wengine wenye taarifa ziada juu ya ukweli wa matukio yanayofanyiwa uchunguzi katika Ghaza.