Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

BU lapitisha azimio kuidhinisha MONUC kutumia "nyenzo zote za lazima" kuwahami raia katika JKK

Ijumatano wajumbe wa Baraza la Usalama (BU), wanaowakilisha mataifa wanachama 15, walipitisha, kwa kauli moja, azimio lenye kuruhusu Vikosi vya Ulinzi Amani vya UM katika JKK (MONUC), kutumia "uwezo wote walionao", chini ya Mlango wa VII wa Mkataba wa UM, unaoruhusu kutumia nguvu, ili kuwapatia raia hifadhi wanayostahiki, dhidi ya mashambulio kutoka makundi yote yenye kuhatarisha usalama wao.

Hapa na pale

Baraza Kuu Alkhamisi limepitisha bajeti la UM kwa 2010-2011, linalogharamiwa dola bilioni 5.16, hatua iliopongezwa na KM Ban Ki-moon kwa kukamilishwa kwa wakati. Kwa mujibu wa taaarifa iliotolewa kwa waandishi habari, Msemaji wa KM alisema Mkuu wa UM, binafsi, aliahidi "mchango wa bajeti liliopitishwa

Hapa na pale

Mashirika ya UM yanayohudumia misaada ya kiutu wiki hii yameanza kufarajia vifaa vya kunusuru maisha katika Malawi kaskazini, kufuatia mitetemeko ya ardhi iliopiga huko mwezi huu na kuua watu wanne, kujeruhi watu 300 ziada na kuharibu au kubomoa nyumba karibu 4,000. Wilaya ya Karonga, Malawi kaskazini iliathirika vibaya zaidi kufuatia msururu wa zilzala zilizopiga kuanzia tarehe 06 mpaka 20 Disemba, mitetemeko iliokadiriwa kuvuka vipimo vya baina ya 5.4 na 6.0 Richter, kwa mujibu wa taarifa ya Shrika la UM juuya Misaada ya Dharura (OCHA). Tume ya kiufundi ya pamoja, ikijumuisha watumishi wa shirika la UM juu ya maendeleo ya watoto, UNICEF; miradi ya chakula, WFP; huduma za chakula na kilimo, FAO, pamoja na taasisi juu ya udhibiti wa watu, UNFPA Ijumatano walielekea Karonga kufanya tathmini halisi juu ya mahitaji ya kiutu, hasa yale yanayohusu afya na lishe, maji salama, usafi, vifaa vya ilmu na akiba ya chakula. Mashirika ya UM yanayohudumia misaada ya kiutu yameeleza kushirikiana, kwa ukaribu zaidi, na mashirika yasio ya kiserikali pamoja maofisa wa Seikali ya Malawi katika kusimamia huduma za kufarajia waathirika wa mitetemeko ya ardhi nchini.

Hapa na pale

Terje Roed-Larsen, mjumbe wa UM anayehusika na utekelezaji wa Azimio 1559 (2004) la Baraza la Usalama, ameripotiwa na Msemaji wa KM, Martin Nesirky, kwamba huwa anashauriana mara kwa mara na maofisa wa Lebanon kadha pamoja na washirika wengine wa Ki-Arabu katika eneo, na vile huwa anashauriana na mataifa yote mengine yanayohusika na utekelezaji wa azimio hilo la Baraza la Usalama. Taarifa hii ilitolewa kujibu suala kujua nani hushirikiana na mjumbe wa UM juu ya utekelezaji wa Azimio husika. Azimio 1559 la Baraza la Usalama lilipopitishwa 2004 lilikusudiwa hasa kuunga mkono pendekezo la kufanyisha uchaguzi wa uraisi Lebanon, ulio huru na wa haki; na lilitilia mkazo kuondoshwa kwa “vikosi vya kigeni” viliopo Lebanon, kwa wakati huo, ikimaanisha, kwa lugha ya kidiplomasiya, vikosi vya Syria. Kwa hivi sasa Syria imekataa kabisa kujihusisha, wala kushiriki kwenye mashauriano ya aina yoyote yale yanayosimamiwa na mjumbe wa UM, Terje Roed-Larsen.