Hapa na Pale
Kwenye mkutano wa hadhara, asubuhi, na watumishi wa UM, KM Ban Ki-moon alisema mgogoro uliopamba sasa hivi katika Tarafa ya Ghaza, na pia Israel kusini, umesasbabisha uharibifu zaidi katika saa 48 zilizopita. Alisema mateso na maumivu yaliowakumba raia yanashtusha, na alisisitiza operesheni za vikosi vya Israel zilizoanzishwa Ijumamosi ndani ya Ghaza yenyewe, zimeharibu kabisa hali katika eneo hilo.~