Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mkuu wa MONUC akumbusha, vikosi vya UM katika JKK huhami maelfu ya raia kila siku

Alan Doss, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK), na pia Mkuu wa Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika JKK (MONUC) kwenye makala aliochapisha mapema wiki hii, katika gazeti la kila siku la Marekani linaloitwa The Washington Times, alieleza kwamba UM huchangisha pakubwa katika kuwatekelezea haki za kimsingi, takriban kila siku, kwa maelfu ya raia wanaoishi kwenye mazingira ya wasiwasi ya JKK.

Hapa na pale

Alan Doss, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK), na pia Mkuu wa Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika JKK (MONUC) leo alichapisha kwenye gazeti la kila siku la Marekani, linaloitwa The Washington Times, insha yenye maelezo maalumu yaliokumbusha mchango wa kila siku wa UM, katika kuwatekelezea maelfu ya raia haki zao za kimsingi, kwenye mazingira ya

Hekaheka za Mkutano wa COP15 zazingatiwa na mtaalamu wa kimazingira kutoka Tanzania

Majadiliano ya Mkutano Mkuu wa Copenhagen, au Mkutano wa COP15, uliofanyika mwezi Disemba, na yaliochukua wiki mbili, yalipambwa na michuano, mivutano na mabishano yasiotarajiwa juu ya itifaki ya kuzingatiwa na wajumbe wa kimataifa, ili kuimarisha kipamoja Mkataba wa Kyoto, na kuyasaidia Mataifa Wanachama kuwa na chombo cha sheria ya kudhibiti bora athari zinazozalishwa na hali ya hewa ya kigeugeu.