Mkuu wa MONUC akumbusha, vikosi vya UM katika JKK huhami maelfu ya raia kila siku
Alan Doss, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK), na pia Mkuu wa Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika JKK (MONUC) kwenye makala aliochapisha mapema wiki hii, katika gazeti la kila siku la Marekani linaloitwa The Washington Times, alieleza kwamba UM huchangisha pakubwa katika kuwatekelezea haki za kimsingi, takriban kila siku, kwa maelfu ya raia wanaoishi kwenye mazingira ya wasiwasi ya JKK.