Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNEP itaisaidia Yemen kitaaluma, kwa kupitia mtandao, kudhibiti mazingira nchini

Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) limetangaza kuwa litaipatia Yemen fursa ya kupokea makala muhimu za kisayansi, kwa kutumia taratibu za mtandao, ikiwa miongoni mwa miradi ya kujiendeleza na maarifa ya sayansi ya kisasa kwenye nchi zinazoendelea, katika kipindi ambacho mataifa haya huwa yanakabiliwa na matatizo kadha wa kadha, yanayozushwa na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

UNAMID/Sudan waahidi ushirikiano kuimarisha usalama Darfur

Wawakilishi wa Shirika la Vikosi vya Mchanganyiko vya UM-UA kwa Darfur (UNAMID) pamoja na wawakilishi wa Serikali ya Sudan wameripotiwa kutiliana sahihi makubaliano ya jumla, kuhusu mradi wa utendaji, uliokusudiwa kuhakikisha watumishi wa UNAMID pamoja na mali zao, huwa watapatiwa usalama wanaostahiki kwenye jimbo la mvutano la Sudan Magharibi la Darfur.

Hapa na pale

Ijumanne, wawakilishi wa kutoka Shirika la Vikosi vya Mchanganyiko vya UM-UA kwa Darfur (UNAMID) walitiliana sahihi na Serikali ya Sudan makubaliano ya jumla kuhusu mradi wa utendaji, uliokusudiwa kuhakikisha usalama wa watumishi wa UNAMID pamoja na mali zao. Taadhima ya utiaji sahihi mapatano haya ilifanyika kufuatilia kikao cha utendaji kazi, kilichokutana Khartoum Ijumapili ya tarehe