Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Paulina Ajello mfanyakazi wa WHO kitengo cha mawasiliano na ushirikishaji jamii akizungumza na wanajamii waelimishaji kuhusu Ebola.
Picha: WHO_Uganda/PhilipKairu

Jiji la Kampala laendesha kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Ebola

Wakati huu ambapo hakuna mgonjwa mpya wa Ebola aliyesajiliwa katika mji mkuu wa Uganda tangu tarehe 14 Novemba, 2022 mamlaka ya afya ya Mji Mkuu wa Kampala kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ya nchi hiyo hivi karibuni ilifanya kampeni ya siku saba kuelimisha umma ili kudumisha umakini wa watu na hatimaye kusaidia kumaliza mlipuko wa ugonjwa huo hatari duniani.

Hali ya hewa na majanga kama mafuriko makubwa, joto na ukame viliathiri mamilioni ya watu na kugharimu mabilioni mwaka 2022, wakati ishara za hadithi na athari za mabadiliko ya hali ya hewa zikiongezeka.
© WMO/Kureng Dapel

Majanga ya tabianchi na hali ya hewa 2022 yandhihirisha haja ya kuchukua hatua zaidi: WMO

Masuala ya hali ya hewa, maji na majanga yanayohusiana na tabianchi, ikiwa ni pamoja na mafuriko makubwa, joto na ukame vimeathiri mamilioni ya watu na kugharimu mabilioni ya dola mwaka huu, huku ishara na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayochochewa na binadamu vikiongezeka kwa mujibu wa taarifa ya tathimini iliyotolewa leo na shirika la umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO.

Wasichana wadogo katika kambi ya wakimbizi wa ndani nchini Myanmar wanachota maji kutoka kwenye kisima.
UNOCHA/Z. Nurmukhambetova

Azimio dhidi ya Myanmar lisiwe maneno matupu; Mtaalamu wa UN aliambia Baraza la Usalama

Siku moja baada  ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio kuhusu Myamar kwenye mkutano wake uliojadili hali ya amani na usalama nchini humo, Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Myanmar Tom Andrews amesema azimio hilo la kusitisha uhasama na kurejesha utawala wa kidemokrasia halitakuwa na maana lisipotekelezwa kwa vitendo.