Sabrina Elba, Balozi mwema wa IFAD, aona jinsi miradi yanufaisha vijana kaunti ya Nyeri Kenya
Mabadiliko ya tabianchi yanayoendelea kukumba Dunia kila uchao hayajaacha wakulima salama. Nchini Kenya, wakulima vijana katika kaunti ya Nyeri, miaka miwili iliyopita walitegemea mto wa jirani na maji ya mvua kumwagilia mashamba yao ya mboga za majani. Hata hivyo ukame na mvua zisizotabirika vilivyosababishwa na mabadiliko ya tabianchi vilikatisha wakulima tamaa.