Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNICEF

Wanafunzi wapatiwa elimu ya namna ya kuishi na watu wenye ualbino

Mtoto umleavyo ndio akuavyo ni methali unaofundisha jamii kuhakikisha iwapo inataka watoto wawe na tabia fulani basi ni vyema waanze kuwafundisha wangali wadogo. Na ndicho kinachofanywa nchini Tanzania na Chama cha watu wenye ualbino TAS mkoa wa Morogoro, mashariki mwa taifa hilo. 

Chama hicho kinaendelesha programu ya kutoa elimu kwa wanafunzi na kimetembelea shule ya msingi kilakala iliyopo Manispaa ya Morogoro na kutoa elimu kwa wanafunzi wa darasa la sita na la saba juu ualbino na namna ya kuishi nao katika Jamii.

Sauti
3'23"
UN News

FAO Tanzania waadhimisha siku ya unywaji maziwa shuleni kwa kutoa maziwa kwa shule za msingi

Leo ni siku ya Kimataifa ya unywaji maziwa shuleni, siku inayopigiwa chepuo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo duniani FAO na kauli mbiu ya mwaka huu ni "Faulu Mtihani kwa glasi moja ya maziwa kila siku". FAO inasema unywaji wa kila siku wa kikombe cha maziwa ya ng’ombe cha ujazo wa mililita 200 humpatia mtoto mwenye umri wa miaka mitano asilimia 21 ya mahitaji ya protini na virutubisho vingine vya madini kama vile Kalsiamu, Magnesiamu na Vitamini. Kwa muj

Sauti
3'55"
UN/Anold Kayanda

Ni lazima kwanza viongozi wayafahamu matatizo ya elimu ni ni yapi ndipo tuyatatue- Cherinet Harifo

Leo mkutano wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu umekunja jamvi. Mmoja wa waliohudhuria ni kijana Cherinet Harifo kutoka Tigray Ethiopia ambaye katika mkutano huu ameziwakilisha nchi mbili, Ethiopia na Eritrea. Yeye msimamo wake ni kwamba, ili kutatua matatizo ya elimu, ni muhimu kwanza viongozi wafahamu matatizo yenyewe ni yapi kwa kila nchi na eneo kwani kila sehemu ina matatizo yake mahususi. Nahicho ndicho kimemleta katika mkutano huu. Kupitia makala hii, kijana huyo anaeleza changamoto zizoikabili nchi yake na nchi jirani ya Eritrea.

Sauti
3'47"
© UNICEF/Yves Nijimbere

Huduma ya RapidPro iliyoletwa na UNICEF imeokoa watoto wetu Turkana nchini Kenya – Wazazi

Kaunti ya Turkana nchini Kenya inakabiliwa na ukame wa muda mrefu. Ili kusaidia kuimarisha mifumo ya lishe, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, nchini Kenya limeanzisha mfumo wa simu za mkononi uitwao RapidPro. Huduma hii huwezesha vituo vya afya kushirikishana ujumbe wa lishe na wafanyakazi wa kujitolea wa afya ya jamii, ambao huripoti taarifa na takwimu mbalimbali za kiafya kuhusu jamii zao. 

Sauti
3'45"
UNCDF

Ushirikiano wa UNCDF na wananchi wa Ikungi Tanzania waleta mabadiliko chanya

Kuanzia wiki hii viongozi wa ulimwengu wanamiminika jijini New York Marekani kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kushiriki Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Mambo kadhaa yatajadiliwa ikiwemo amani, haki za binadamu, uchumi na kuilinda sayari dunia dhidi ya uharibifu unaochochea majanga. Ulimwengu tayari umebaini kuwa changamoto zimefungana na hivyo majawabu yanapaswa kutafutwa kwa kushirikiana. Katika maeneo ambayo ushirikiano umefanyika ili kutafuta ufumbuzi wa jambo, matunda yameonekana.

Sauti
4'3"
UNCDF

Ufadhili wa UNCDF umetukwamua sana Kibondo Big Power Group

 

Kibondo Big Power Group (KBPG) ni ushirika wa kilimo mkoani Kigoma, kaskazini magharibi mwa Tanzania. Shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa, UNCDF lilisaidia KBPG kwa msaada wa kifedha ambao ulitumika kupanua shughuli zake kwa kufanya shughuli zifuatazo: kuchimba kisima cha maji mita 100, ununuzi wa pampu ya maji ya jua na ujenzi wa ghala na nyumba za kukausha jua za mihogo na chanja na mtaji wa kufanyia kazi. Hamad Rashid wa redio washirika  Hamad Rashid wa redio washirika wa Redio washirika wetu MVIWATA FM ya mkoani Morogoro, Tanzania anasimulia zaidi.

Sauti
3'52"
Photo: MINUSCA/Honorine Guehi Niare Yao

Kamati ya ulinzi kutoka Bunge la Tanzania yazuru shughuli za MINUSMA

Kamati ya kudumu ya ulinzi na usalama ya Bunge la Tanzania imefanya ziara nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ili kujionea shughuli za ulinzi wa amani zinazotekelezwa na vikosi vya nchi mbalimbali kupitia ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA. Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazochangia ulinzi wa amani kwa kupeleka wanajeshi walinda amnai ambapo kwa sasa kikosi kinachohudumu nchini CAR ni kikosi cha 5 kutoka tangu Tanzania ilipanza kupeleka walinda amani nchini humo ili kusaidia kulinda raia na kusimamia amani.

Sauti
3'30"
UN Video

Najivunia ufadhili wa MONUSCO umeniwezesha kuwasaidia wenzangu:Jafari DRC

Kutana na Alex Safari kutoka Goma mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, mtaalamu huyu wa kutengeneza simu DRC ambaye kwa msaada wa mpango wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO aliweza kupatia mafunzo au formation[FORMASSION]  kwa lugha ya kifaransa, vijana wa kike na wa kiume, wakiwemo waliotumikishwa vitani , mafunzo ambayo sio tu yaliwaepusha kujihusisha na vita na kuzurura mitaani bali yamebadili maisha yao. Assumpta Massoi alifika kitongoji cha Majengo jimboni humo  ku

Sauti
3'17"