Wanafunzi wapatiwa elimu ya namna ya kuishi na watu wenye ualbino
Mtoto umleavyo ndio akuavyo ni methali unaofundisha jamii kuhakikisha iwapo inataka watoto wawe na tabia fulani basi ni vyema waanze kuwafundisha wangali wadogo. Na ndicho kinachofanywa nchini Tanzania na Chama cha watu wenye ualbino TAS mkoa wa Morogoro, mashariki mwa taifa hilo.
Chama hicho kinaendelesha programu ya kutoa elimu kwa wanafunzi na kimetembelea shule ya msingi kilakala iliyopo Manispaa ya Morogoro na kutoa elimu kwa wanafunzi wa darasa la sita na la saba juu ualbino na namna ya kuishi nao katika Jamii.