Mazungumzo ya Afrika katika UN yaanza leo New York, Elimu kumulikwa
Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vimeanza vikao vya wiki tatu kuhusu Mazungumzo kuhusu Afrika au ADS2024 maudhui yakiwa Elimu kupitia Sayansi, Teknolojia na Ugunduzi kuelekea Afrika Tuitakayo.