Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watu wakichota maji ya kunywa huko Rafah kusini mwa Gaza
© UNRWA

Gaza: Huko Rafah hofu yatanda, wagonjwa wahofia kusaka huduma

Hofu kubwa ikiendelea kutanda huko Rafah, kusini mwa Gaza wakati huu ikiripotiwa kuwa Israel inataka kuelekeza operesheni zake za kijeshi kwenye eneo hilo, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni ,WHO linasema hospitali tayari zimezidiwa uwezo kwani Umoja wa Mataifa umekuwa unasema operesheni hiyo ya kijeshi itasababisha idadi kubwa ya vifo na majeruhi ambao watahitaji huduma za afya.