Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanafunzi wa Mauritania waliporejea shuleni baada ya miezi kadhaa ya shule kufungwa kutokana na COVID-19
© UNICEF/Raphael Pouget

Virusi vilivyoufunga ulimwengu: Elimu katika janga

Watoto ulimwenguni kote masomo yao yamevurugika sana mwaka huu, kwani shule zinajitahidi kukabiliana na hali ya kufungwa na kufunguliwa tena kwa shule, na kuelekea katika masomo ya mtandaoni ikiwa hata ni chaguo. Watoto walio katika hali duni, hata hivyo, wameathirika zaidi na hatua za dharura zilizochukuliwa. Katika sehemu ya tatu ya tathimini yetu ya athari ya COVID-19 kwa ulimwengu, tunajikita kwenye janga la elimu lililosababishwa na janga la COVID-19.

Mhudumu wa afya akisambaza vifaa vya kujisafi kwa familia moj ahuko Dhaka, mji mkuu wa Bangladesh
UN Women/Fahad Kaizer

Virusi vilivyofunga dunia: Pengo linalopanuka kati ya matajiri na maskini

Wakati wa janga la COVID-19 pengo la ukosefu wa usawa kati ya matajiri na maskini limeongezeka zaidi, halikadhalika umaskini, ikiwa ni mara ya kwanza katika miongo kadhaa. Katika sehemu hii ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu jinsi COVID-19 imebadili dunia, tunaangazia jinsi janga hilo limerudisha nyuma juhudi za kujenga jamii zenye usawa zaidi. 

Mradi wa FAO wa uhakika wa chakula (PESA) katika sekta ya kilimo, mifugo, maendeleo vijijini, uvuvi na kilimo
© FAO-Magnum Photos/Alex Webb

FAO yakidhi kiu ya wafugaji na wakulima huko Togo

Maji ni hai ni kauli ambayo imethibitika kwa wakazi wa jimbo la Dankpen nchini Togo, baada ya Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na kilimo, FAO na serikali, kukarabati bwawa linalotumika hivi sasa kwa shughuli siyo tu za umwagiliaji, bali pia maji kwa wanyama na utalii.

Sauti
1'55"