Udhibiti wa COVID-19 usiingilie mnyororo wa usambazaji wa chakula-FAO, WHO, WTO
Mashirika ya Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo duniani, FAO, la afya WHO na lile la biashara duniani yamesema mamilioni ya watu ulimwenguni kote hutegemea biashara ya kimataifa kwa uhakika wao wa chakula na riziki. Wakati nchi zinachukua hatua za kudhibiti janga la virusi vya corona, COVID-19, ni lazima kuwa makini ili kupunguza athari zinazoweza kupatikana katika usambazaji wa chakula au matokeo yasiyotarajiwa katika biashara ya kimataifa na usalama wa chakula.