Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Umoja wa Mataifa na harakati za kusaidia kuhakikisha uhakika wa chakula.
IFAD/GMB Akash

Udhibiti wa COVID-19 usiingilie mnyororo wa usambazaji wa chakula-FAO, WHO, WTO

Mashirika ya Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo duniani, FAO, la afya WHO na lile la biashara duniani yamesema mamilioni ya watu ulimwenguni kote hutegemea biashara ya kimataifa kwa uhakika wao wa chakula na riziki. Wakati nchi zinachukua hatua za kudhibiti janga la virusi vya corona, COVID-19, ni lazima kuwa makini ili kupunguza athari zinazoweza kupatikana katika usambazaji wa chakula au matokeo yasiyotarajiwa katika biashara ya kimataifa na usalama wa chakula.

Wakimbizi wa ndani walio katika jimbo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC
© UNFPA DRC

Haki na afya ya wakimbizi, wahamiaji na wasio na utaifa inatakiwa kulindwa wakati wa kushughulikia COVID-19

Taarifa ya pamoja kwa vyombo vya habari iliyotolewa hii leo na Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la wahamiaji, IOM, la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la afya WHO imetoa wito kwa dunia kulinda haki na afya ya wakimbizi, wahamiaji na wasio na utaifa katika wakati huu wa mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19.

Bendera za Umoja wa Mataifa na ile ya Olimpiki zikiwa zinapepea kwa pamoja kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN/Eskinder Debebe

COVID-19 yasababisha Olimpiki kusogezwa mwaka mmoja mbele, sasa kuchezwa 2021

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki IOC na Kamati ya kimataifa ya Paralimpiki IPC au Olimpiki ya watu wenye ulemavu, kwa pamoja kamati ya maandalizi ya Tokyo 2020, Serikali ya mji wa Tokyo na serikali ya Japani wametangaza kuwa kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19, sasa michezo ya Olimpiki iliyokuwa ifanyike mwaka huu mjini Tokyo, itafanyika mwaka ujao wa 2021.

Sauti
3'24"
Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni.
UN News/ UNIC Tanzania

COVID-19: Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni

Ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ukiwa umeshasambaa katika mataifa 199 ikiwemo Tanzania, vijana nao wanaibuka na ubunifu mbalimbali ili kusaidia mataifa yao katika kudhibiti kuenea kwa gonjwa hilo lisilo na tiba wala chanjo. Ubunifu wa vifaa vya kudhibiti kuenea umefanywa na kijana mmoja nchini Tanzania kama anavyoripoti… wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam.

Sauti
2'