Dola bilioni 9 za kimarekani kutoka tumbaku zinatumika kuwavutia vijana kujaza nafasi ya wanaouawa na bidhaa hiyo kila mwaka-WHO
Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kimataifa ya kutovuta tumbaku, siku inayoadhimishwa kila tarehe 31 mwezi Mei ili kukuza uelewa kuhusu madhara ya zao hilo, shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linaeleza kuwa kila mwaka tasnia ya tumbaku inawekeza zaidi ya dola bilioni 9 za kimarekani kutangaza bidhaa zake zaidi ikiwalenga vijana na nikotini na tumbaku kwa nia ya kujaza nafasi ya watu milioni 8 ambao bidhaa hiyo inawaua kila mwaka.