Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

WHO inatoa wito kwa vijana wote kuungana kupigana na Tumbaku ili kuwa kizazi kisicho tumia tumbaku.
WHO

Dola bilioni 9 za kimarekani kutoka tumbaku zinatumika kuwavutia vijana kujaza nafasi ya wanaouawa na bidhaa hiyo kila mwaka-WHO

Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kimataifa ya kutovuta tumbaku, siku inayoadhimishwa kila tarehe 31 mwezi Mei ili kukuza uelewa kuhusu madhara ya zao hilo, shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linaeleza kuwa kila mwaka tasnia ya tumbaku inawekeza zaidi ya dola bilioni 9 za kimarekani kutangaza bidhaa zake zaidi ikiwalenga vijana na nikotini na tumbaku kwa nia ya kujaza nafasi ya watu milioni 8 ambao bidhaa hiyo inawaua kila mwaka.

Programu za misaada ya chakula nchini Chad zinakuza kilimo endelevu na inaimarisha kipato na riziki.
WFP/Giulio d'Adamo

Vita dhidi ya COVID-19 na utimizaji wa SDGs ni mitihani inayohitaji fedha:UN

Mkutano wa ngazi ya juu wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo umefanyika leo Alhamisi ukihusisha Umoja wa Mataifa  na maafisa wawakilishi wa serikali mbalimbali, lengo kubwa likiwa ni kuchagiza msaada wa kimataifa wa fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi zinazoendelea ambazo zimedhoofishwa Zaidi na mlipuko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 katika katika hatua zake za utumizaji wa malengo ya maendeleo endelevu , SDGs.