Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watu wakiwa wamevalia vifaa vya kujikinga katika eneo la kusubiri katika uwanja wa ndege wa Shenzhen Bao'an wa kimataifa.
UN News/Jing Zhang

Tuko tayari kusaidia kiufundi katika mlipuko wa corona:IOM

Wakati hofu ikiendelea kutanda kuhusu idadi ya visa vilivyoripotiwa kutokana na mlipuko wa virusi vipya vya Corona na pia kusambaa kwake katika nchi 18 hivi sasa, shirika la umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema liko tayari kutoa msaada wa kiufundi kwa serikali likishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO ili kuwawezesha watu kusafiri katika njia salama kiafya na kusaidia utekelezaji wa hatua za afya za kijamii ili kuhakikisha athari ndogo katika jamii na uchumi.

Muuguzi akiandaa chanjo ya kuchanja mtoto katika kliniki Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Thomas Nybo

Mikakati ya kupambana na homa ya manjano, Uganda

Uganda, imeimarisha juhudi za kudhibiti mlipuko wa homa ya manjano kaskazini magharini na magharibi ya kati mwa nchi wakati huu ambapo tayari watu wanne wameaga dunia kutokana na mpuko wa homa ya njano kama anavyosimulia mwandishi wetu John Kibego katika ripoti ifuatayo.

Sauti
2'44"
Abiria wakiwa wamejikinga na maambukizi ya mfumo wa hewa wakiwa katika treni za chini ya ardhi huko Shenzhen China
UN News/Jing Zhang

Virusi vya Corona sasa vyatangazwa kuwa dharura ya kiafya ya kimataifa

Mkutano wa pili wa kamati ya dharura ulioitishwa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la afya duniani, WHO, chini ya sheria za kimataifa za afya (IHR) (2015) kuhusiana na mlipuko wa virusi vya corona 2019-nCoV nchini China, umeutangaza mlipuko huowa virusi vya corona kuwa ni dharura ya kiafya ya kimataifa, PHEIC.