Vikwazo vya ununuzi wa silaha vinaendelea CAR-Baraza la usalama
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa hii leo tarehe 31 limepitisha azimio lilowasilishwa na Ufaransa kuendelea kuiweka vikwazo vya ununuzi ya silaha Jamhuri ya Afrika ya kati.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa hii leo tarehe 31 limepitisha azimio lilowasilishwa na Ufaransa kuendelea kuiweka vikwazo vya ununuzi ya silaha Jamhuri ya Afrika ya kati.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limekaribisha sheria mpya iliyopitishwa nchini Tajikistan ambayo inaruhusu raia wa kigeni na watu wasio na utaifa wanaoishi nchini humo kuhalalisha ukaaji wao kwa kupata vibali vya kuishi moja kwa moja ambavyo vitawawezesha pia baada ya miaka mitatu kuomba uraia wa Tajikistan.
Wakati hofu ikiendelea kutanda kuhusu idadi ya visa vilivyoripotiwa kutokana na mlipuko wa virusi vipya vya Corona na pia kusambaa kwake katika nchi 18 hivi sasa, shirika la umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema liko tayari kutoa msaada wa kiufundi kwa serikali likishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO ili kuwawezesha watu kusafiri katika njia salama kiafya na kusaidia utekelezaji wa hatua za afya za kijamii ili kuhakikisha athari ndogo katika jamii na uchumi.
Uganda, imeimarisha juhudi za kudhibiti mlipuko wa homa ya manjano kaskazini magharini na magharibi ya kati mwa nchi wakati huu ambapo tayari watu wanne wameaga dunia kutokana na mpuko wa homa ya njano kama anavyosimulia mwandishi wetu John Kibego katika ripoti ifuatayo.
Mlipuko wa nzige wa jangwani unaendelea kuwa mbaya na ni tishio kubwa kwa uhakika wa chakula na mbinu za kujipata kipato katika Pembe ya Afrika.
Shirika la afya ulimwenguni WHO limeendelea kuzitaka nchi zote kuchukua tahadhari na kujiandaa dhidi ya virusi vya corona ambavyo tayari vimetangazwa kuwa dharura ya afya ya kimataifa vitazuka katika nchi zao.
Mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu mzozo wa Israeli na Palestina ni pendekezo linaloegemea kabisa katika upande mmoja kwa mzozo huo, amesema Michael Lynk, mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa juu ya hali ya haki za binadamu katika eneo la Palestina linalokaliwa tangu mwaka 1967.
Mkutano wa pili wa kamati ya dharura ulioitishwa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la afya duniani, WHO, chini ya sheria za kimataifa za afya (IHR) (2015) kuhusiana na mlipuko wa virusi vya corona 2019-nCoV nchini China, umeutangaza mlipuko huowa virusi vya corona kuwa ni dharura ya kiafya ya kimataifa, PHEIC.
Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Libya na mkuu wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNSMIL amesema anasikitika kwamba makubaliano ya Berlin ya usitishaji uhasama nchini Libya yanatekelezwa kwa jina tu na si kwa vitendo.
Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq na mkuu wa mpango wa Umoja huo UNAMI amesema kuendelea kupotea kwa Maisha ya vijana na umwagaji damu wa kila siku ni hali ambayo haiwezi kuvumilika nchini humo.