Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kituo cha udhibiti wa magonjwa, CDC, nchini  Marekani kimeanza operesheni zake za dharura kusaidia wadau wa afya katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona duniani.
CDC/James Gathany

Corona isituchanganye, tuchukue hatua; Syria nako ni janga linalotia shaka zaidi- Guterres

Makombora yakizidi kumiminikia raia wasio na hatia nchini Syria, huku virusi vya Corona navyo vikizidi kusambaa maeneo mbalimbali duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari na kuhusu zahma hizo akisema  kuwa kwa Corona huu si wakati wa kuchanganyikiwa na kwa Syria, janga hilo ni moja ya mazingira ya kutia shaka zaidi kwenye muongo wa sasa.

Syria
OCHA Syria

Maelfu ya watu Maisha yao yanaendelea kuwa hatarini Syria:WHO/OCHA/UNHCR

Umoja wa Mataifa unaendelea kufuatilia kwa karibu hali inayotia hofu kubwa Kaskazini Magharibi mwa Syria kufuatia taarifa kwamba askari kadhaa wa Uturuki wameuawa kwenye shambulio la anga. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejelea wito wake wa kusitisha uhasama mara moja na kuokoa Maisha ya raia walio hatarini kufiuatia machafuko yanayoendelea na mashambulizi.

Sauti
2'22"
Vipimo vya virusi vya ukimwi.
Public Health Alliance/Ukraine

Wanawake wanaoishi wa HIV wanalazimishwa kuwa tasa na kutoa mimba:UNAIDS

Wanawake wanaoishi na virusi vya ukimwi VVU kote duniani wamekuwa wakipambana  kwa miongo ili kutambuliwa haki zao za afya ya uzazi ikiwemo haki ya kuanza familia na kuwa na watoto. Lakini kwa mujibu wa taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na UKIMWI, UNAIDS kumekuwa na mifano mingi ya wanawake hao kulazimishwa kutozaa na kutoa mimba.