Tunatuma salamu za sikukuu kwa raia wa CAR na tunawatakia mwaka mpya wenye amani - TANBAT 5
Katika kuelekea kuukamilisha mwaka 2021 na kuingia katika mwaka mpya wa 2022, Walinda amani wa Kikosi cha 5 cha Tanzania kinacholinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, TANBAT 5 wametuma salamu za kuwatakia msimu wa sikukuu za Krismasi na mwisho wa mwaka raia wanaowalinda.