Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Familia ya watu waliohamishwa makazi yao huko Tabarre, Haiti wakusanyika kwenye tovuti.
© UNICEF/Ndiaga Seck

UNICEF: Watoto 170,000 nchini Haiti wafurushwa makwao

Wakati mzozo wa makundi yanayotumia silaha uliendelea kuongezeka nchini Haiti, shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF hii leo limeeleza idadi ya watoto waliokimbia makazi yao imefikia 170,000 na kutaja kuwa hiyo ni idadi kubwa ya kutisha inayoashirikia kuzidi kuzorota kwa usalama nchini humo huku watoto na familia zao wakizidi kuwa hatarini. 

Ujenzi wa madarasa nchini Mozambique yanayohimili hali mbaya za hewa ikiwemo vimbunga vinavyong’oa mapaa.
UN Habitat Mozambique

Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama: Mwanafunzi Msumbiji

Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni  hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora. 

Sauti
4'11"
Timu za UNRWA zinafanya kazi usiku kucha kusambaza chakula kwa Wapalestina waliokata tamaa.
© UNRWA

'Hatuwezi kuwatelekeza watu wa Gaza': wakuu wa mashirika ya UN na mashirika yasiyo ya kiserikali

Wakati mapigano makali na mashambulizi ya makombora yaliendelea huko Khan Younis kusini mwa Gaza usiku wa kuamkia leo Jumatano, wasaidizi wakuu wa Umoja wa Mataifa na wakuu wa mashirika yasiyo ya kiserikali wameonya juu ya ‘matokeo mabaya’ ya kutofadhili shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ambalo linashutumiwa kushirikiana na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas.

 Sigrid Kaag, Mratibu Mwandamizi wa Masuala ya Kibinadamu na Ujenzi mpya wa Gaza akitoa maelezo kwa wanahabari kufuatia mashauriano na Baraza la Usalama.
UN Photo/Manuel Elías

'Hakuna mbadala' wa kazi ya UNRWA kuokoa maisha huko Gaza - Sigrid Kaag

Hakuna shirika linaloweza kuchukua nafasi ya shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, katika Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita, Mratibu Mwandamizi wa Masuala ya Kibinadamu na Ujenzi mpya wa Gaza Sigrid Kaag amewaeleza waandishi wa habari leo Januari 30 nje ya Baraza la Usalama katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa.  

Wakazi wakisubiri kufanyiwa uchunguzi wa ugonjwa wa Lymphatic Filariasis na Onchocerciasis huko Muheza, Tanzania.
© CDC Global Health

Kwa hatua madhubuti twaweza kiutokomeza NTDs: WHO

Leo ni siku ni siku ya magonjwa ya kitropiki yaliyopuuzwa duniani. Katika ujumbe wake wa siku hii Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema, “Magonjwa ya kitropic yaliyopuuzwa au NTDs yanaathiri zaidi ya watu bilioni moja duniani kote hususani katika jamii masikini na zilizotengwa, lakini magonjwa ya NTDs yanazuilika na mara nyingi yanaweza kutokomezwa kabisa katika nchi.”

Wapalestina wakiwa kwenye foleni ya kutafuta chakula kwenye mvua kwenye makazi huko Deir Al-Balah, Gaza.
© UNRWA

Mgogoro wa ufadhili UNWRA ukiendelea raia Gaza wapekua malori kusaka mlo

Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ankukutana na wawakilishi kutoka nchi zinazotoa misaada kwa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA kufuatia madai ya baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo kushirikiana na Hamas, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, leo limesema sasa si wakati wa kuwatelekeza watu wa Gaza.