Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mlinda amani kutoka Timu ya kuwahusisha wanawake ya MONUSCO akisambaza barakoa katika kijiji cha Walungu nchini DR Congo
MONUSCO

DNA za walinda amani wa Afrika Kusini huko DRC zakusanywa kubaini baba za watoto 

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, jeshi la Afrika Kusini limepeleka timu yake kwenye  ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO,ili kuchunguza vijinasaba vya watoto na wanawake waliobakwa na walinda amani ili hatimaye kuthibitisha iwapo watuhumiwa ni walinda amani kutoka Afrika Kusini na kisha watoto hao watambue baba zao na pia kupatiwa malezi. 

Sauti
2'39"
Wasichana wakijifunza masuala ya kuvunja ungo na hedhi kwenye darasa la wasichana pekee lililo chini ya mradi wa Umoja wa Mataifa huko Bol nchini Chad.
UN/Eskinder Debebe

Je suala la kukata hedhi lipatiwe kipaumbele pahala pa kazi? 

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na ajira duniani, ILO limeanzisha mjadala wa kuangazia iwapo suala la mwanamke kukata hedhi ni suala linalopaswa kuangaziwa pahala pa kazi baada ya utafiti uliofanyika nchini Uingereza kubaini kuwa changamoto za kiafya zitokanazo na kukatika kwa hedhi zinasababisha baadhi ya wanawake kushindwa kufanya kazi ipasavyo na wengine kuamua kuacha kazi hali inayowaathiri kiuchumi.