UNICEF yatoa msaada wa dharura wa chakula kwa watoto nchini Uingereza
Maelfu ya familia zilizoathirika na janga la corona au COVID-19 nchini Uingereza zitapokea msaada wa dharura wa chakula kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika kipindi cha sikukuu na zaidi limetangaza shirika hilo likiongeza kuwa msaada huo utakuwa ni wa mara moja tu.