Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wakimbizi nchini Mauritani wamerejea shule baada ya kufunguliwa baada ya miezi kadhaa kufuatia kuzuka kwa COVID-19.
© UNICEF/Raphael Pouget

COVID-19 inaongezeka Afrika, hatua thabiti zinahitajika-WHO

Maambuki ya COVID-19 katika ukanda wa Afrika yameongezeka kwa kasi katika miezi miwili iliyopita, hali hiyo ikisisitiza hitaji la hatua za afya za umma zilizoimarishwa ili kuzuia kuongezeka kwa maambukizi, hasa wakati watu wanapokusanyika au kusafiri kwa sherehe za mwisho wa mwaka, imeeleza taarifa ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, iliyotolewa hii leo mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo.

Mtoto mkimbizi kutoka Syria akiwa kwenye makazi ya muda nchini Lebanon.
UNICEF/ Dar Al Mussawir

Majira ya baridi yameanza Lebanon wakimbizi wahaha huku ukata ukizidisha adha:UNHCR 

Maelfu ya wakimbizi nchini Lebanon sasa wanaanza kuhaha kwani majira ya baridi yamewadia na kila mwaka huwapa changamoto kubwa lakini mwaka huu madhila yanatarajiwa kuongezeka kutokana na mgogoro wa kiuchumi na mfumoko wa bei ulioanza Oktoba mwaka 2019 ambao sasa umefikia asilimia 174. Yote haya yanamanisha fedha na msaada wanaopewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR hautokidhi mahitaji.

Sauti
2'26"