Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto hawa katika jimbo la Cabo Delgado, kaskazini mwa Msumbiji wanakabiliwa na janga la ukosefu wa chakula, halikadhalika wako hatarini kukumbwa na magonjwa.
WFP/Falume Bachir

Hali bado ni tete kwa watoto Cabo Delgado

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema takribani watoto 250,000 wamekimbia makazi yao kutokana na ghasia zinazoendelea kwenye jimbo la Cabo Delgado kaskazini mwa Msumbiji na sasa wako hatarini kupata magonwa ya kuambukiza kwa kuwa msimu wa mvua unaanza.

Sauti
1'54"
MINUSCA wametuma vikosi vya polisi katika mji mkuu wa CAR, Bangui na viunga vyake kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na makundi yenye silaha kaskazini magharibi mwa mji.
MINUSCA/Hervé Serefio

Umoja wa Mataifa unafanya juhudi za kuhakikisha uwepo wa amani, CAR ikienda kwenye uchaguzi. 

Msemaji wa Katibiu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Stephan Dujarric akizungumza na waandishi wa habari hii leo mjini New York Marekani kuhusu yaliyojadiliwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, amesema Baraza hilo limejadili kuhusu hali ya kukosekana kwa usalama ncini Jamhuri ya Afrika ya kati huku nchi hiyo ikielekea kwenye uchaguzi. 

Wahamiaji wakiandaa samaki kwa ajili ya mauzo katika soko moja mjini Dubai
ILO/Deloche P

Tunachopitia sasa kwenye COVID-19 wahamiaji hupitia kila uchao- Guterres

Ikiwa leo ni siku ya wahamiaji duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema ni mwaka wa kutathmini jinsi janga la Corona au COVID-19 lilivyosababisha mamilioni ya watu kukumbwa na machungu ya kutengana na familia zao na kutokuwa na uhakika wa ajira, jambo ambalo limewapatia watu hisia halisi ambazo wahamiaji hukumbana nazo kila wakati kwenye maisha yao.