Ongezeko la wakimbizi wa ndani Yemen laitia hofu ICRC
ICRC inahofia ongezeko la wakimbizi wa ndani katika mkoa wa Saada nchini Yemen, wakati huu ambapo majira ya baridi yameshika kasi na kuanza kuathiri maisha ya wakimbizi hao.
ICRC inahofia ongezeko la wakimbizi wa ndani katika mkoa wa Saada nchini Yemen, wakati huu ambapo majira ya baridi yameshika kasi na kuanza kuathiri maisha ya wakimbizi hao.
Umoja wa mataifa hauna mpango wa kuitelekeza Somalia licha ya mazingira magumu yanayoambatana na vitisho na ghasia wanayokabiliana nayo wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu.
Afisa wa idara ya umoja wa mataifa juu ya Misaada ya Dharura (OCHA), Bi Elisabeth Byrs amesema kati ya Disemba 27 mwaka 2009 hadi Januari 5 2010 kumekuwepo na mvua kali huko maeneo ya Kaskazini, Kati na Magharibi mwa Kenya , na kuwathiri watu elfu 30.
Katika operesheni mbili tofauti zilizofanyika jana na leo kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu (ICRC) imesaidia katika kuachiliwa na kusafirishwa kwa wanajeshi sita wa jeshi la Congo waliokuwa wanashikiliwa na makundi yenye silaha katika majimbo ya Kivu ya Kusini na Kaskazini.
Wapiganaji wa kijadi wenye silaha wa kabila la Nuer wamewaua takribani watu 139 kutoka kabila hasimu wao, katika kijiji kimoja kusini mwa Sudan, amesema afisa mmoja wa serikali hii leo.
Vita kubwa huenda ikarejea Sudan Kusini iwapo dunia haitachukua hatua ya kulinda mkataba wa amani ambao ulimaliza moja ya vita kubwa na ya muda mrefu barani Afrika.
Mjumbe Maalumu wa KM juu ya Haki za Watoto Walionaswa kwenye Mapigano. Bi Radhika Coomaraswamy, ameitaka mahakama ya kimataifa ya uhalifu kushughulikia suala la jinsi ya kuwalinda watoto wanaojihusisha kwa njia mbalimbali katika vita.
Leo Januari sita Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP), kwa mara ya kwanza limewakutanisha pamoja jamii, viongozi wa dini, na viongozi wa kijeshi ili kubaini ni kwa njia gani jamii zilizosalia na makovu ya vita zinaweza kuishi pamoja kwa amani mashariki mwa Chad.
Mjumbe Maalumu wa KM juu ya Haki za Watoto Walionaswa kwenye Mapigano atatoa ushahidi mbele ya Mahakama ya Kimataifa juu ya Jinai ya Halaiki (ICC) dhidi ya Thomas Lubanga.
PUMA ambayo ni moja ya makampuni makubwa duniani yanayojihusisha na michezo na Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) wametangaza mshikamano maalumu wa kusaidia viumbe hai duniani na hususani barani Afrika.