Sudan na kundi la JEM wafungua ukurasa mpya wa amani
Serikali ya Sudan na kundi la JEM mapema wiki hii waliamua kufungua ukurasa mpya walipoamua kutia saini makubaliano ya mchakato wa amani mjini Doha Qatar.
Serikali ya Sudan na kundi la JEM mapema wiki hii waliamua kufungua ukurasa mpya walipoamua kutia saini makubaliano ya mchakato wa amani mjini Doha Qatar.
Haiti ambayo imesambaratishwa na tetemeko la ardhi la Januari 12 inahitaji kuwezeshwa ili kuanza tena shughuli ya kukabiliana na ongezeko la maambukizi ya Ukimwi. Baada ya UNAIDS na wizara ya afya na idadi ya watu ya Haiti kutathimin hali halisi, UNAIDS imetoa ripoti iitwayo "kuisaidia Haiti kurejesha uwezo wake wa kupambana na Ukimwi".
Mawaziri wa mazingira kutoka kote duniani wametoa azimio lao la kwanza baada ya muongo mmoja. Katika azimio hilo serikali zao zimeahidi kuongeza juhudi za kimataifa ili kukabiliana na changamoto kubwa za mazingira na zinazorudisha nyuma maendeleo.
Leo Umoja wa Mataifa umeamua kuunga mkono upande wa Switzerland baada ya kiongozi wa Libya Moamar Gadaffi kutoa wito wa kuendesha vita vya Jihad dhidi ya Switzerland.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani Margaret Chan ameonya kwamba matumizi ya tumbaku yanaongezeka sana katika nchi zinazoendelea.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya msaada wa kibinadamu OCHA linasema mapigano ya kikabila yameongezeka sana Sudan Kusini tangu mwezi Desemba 2009 na kuendelea hadi Januari na Februari mwaka huu wa 2010.
Mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na ule wa Afrika kwenye jimbo la Darfur Sudan UNAMID, leo umepokea rasmi helkopta tano kutoka Ethiopia ili kusaidia katika shughuli zake za kulinda amani.
Idadi kubwa ya wanawake waishio na virusi vya HIV kaskazini magharibi mwa Cameroon hivi sasa wanashiriki katika miradi ya kujipatia kipato kupitia vyama vya ushirika kwa msaada wa shirika la kazi duniani ILO.
Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kulinda amani Alain Le Roy amewasili nchini Chad kwa ajili ya mazungumzo, kufuatia ombi la serikali mjini Ndjamena la kutaka vikosi vya Umoja wa Mataifa viondoke nchini humo.
Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 ICTR iliyoko mjini Arusha Tanzania, leo imemuhukumu kwenda jela miaka 25 Luten Kanali Ephrem Setako.