Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kuadhimisha siku ya ukimwi duniani UNICEF yazindua ripoti ya AIDS na watoto

Tarehe mosi Desemba kila mwaka huadhimishwa siku ya ukimwi duniani huku shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya ukimwi UNAIDS, shirika la afya duniani WHO, shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF ,mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa na wadau wa kupambana na ukimwi hutoa tathimini ya hatua zilizopigwa wapi palipo na mapungufu na nini kifanyike kuendelea kunusuru maisha ya watu kutokana na ugonjwa huo hatari usio na tiba hadi sasa.

Mzozo wa kisiasa kikwazo cha kupambana na kipindupindu Haiti

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito wa kupatikana kwa suluhu la haraka kwa mzozo wa kisiasa nchini Haiti baada ya duru ya kwanza ya uchaguzi ulioandaliwa siku ya Jumapili akionya kuwa kuendelea kuwepo kwa ukosefu wa usalama huenda kukahujumu jitihada za kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu nchini humo.