Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UM: zaidi ya ajali asili 3 800 zilitokea muongo ulopita

Idara ya Umoja wa Mataifa ya kujaribu kupunguza maafa imeeleza kwamba mnamo muongo uliyopita kumekuwepo na ajali asili 3 800 zilizosababisha vifo vya watu 780 000. Idara hiyo inakadiria ajali asili hizo zimesababisha uharibifu wa mali wa kiasi cha dola bilioni 960.

UM unashiriki katika mkutano wa kimataifa juu ya Yemen

Mkuu wa masuala ya kisiasa wa Umoja wa Mataifa ataongoza ujumbe kushiriki katika mkutano wa mawaziri wa kimataifa uloanza mjini London siku ya Jumatano juu ya hali huko Yemen, wakati wasi wasi unaongezeka kuhusiana na kuzidi kwa ushawishi wa al-Qaida na makundi mengine yenye itikadi kali katika taifa hilo la Kiarabu.