Afisa wa UM anahimiza mkatati wa kupambana na uharamia Somalia
Naibu Mjumbe Maalum wa UM kwa ajili ya Somalia Charles Petrie ametoa mwito wa kuwepo na mkakati thabiti na mpana wa kupambana na uharamia nje ya pwani ya Somalia, akieleza kwamba kuenea kwa tatizo hilo ni kutokana na kutumia mbinu ya kupambana nao baharini pekee yake.