Kongamano la kimataifa la watu wa asili limemalizika mjini New York kwenye UM
Kongamano la kimataifa kuhusu watu wa asili lililokuwa likiendelea kwenye makao makuu ya UM New York limemalizika leo.
Kongamano la kimataifa kuhusu watu wa asili lililokuwa likiendelea kwenye makao makuu ya UM New York limemalizika leo.
Mshauri maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhsu masuala ya Afrika Cheick Sidi Diarra leo ameelekea , Arusha Tanzania kuhudhuria mkutano wa siku mbili.
Wahamiaji tisa kutoka Afrika ambao wamekuwa wakinyonywa na kudhulimiwa na waajiri wao nchini Italia wamepewa kibali cha muda cha kukaa nchini humo chini kwa mujibu wa sheria za uhamiaji za Italia.
Wahenga walinena ukimkomboa mwanamke umeikomboa jamii na mwanamke huyu kabla hajkamilika lazima apitie usichana.
Kamishina mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Antonio Guterres amezitaka nchi 72 za muungano wa Ulaya kuwa mfano mzuri wa kuwalinda wakimbizi.
Mashirika mawaili ya Umoja wa Mataifa yametoa muongozo mpya kwenye wavuti wa wapi unaweza kupata dawa zilizotengenezwa kwa ajili ya watoto.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linasema mwaka mmoja baada ya machafuko ya bonde la Swat Pakistan maelfu ya waathirika bado wanahangaika kujenga upya maisha yao.
Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura John Holmes ambaye yuko ziarani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo , leo amezuru jimbo la Kivu ya Kusini.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameyataka mataifa yote kuiunga mkono mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC iliyoko The Hague Uholanzi.
Kongamano la kimataifa litafanya kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa wiki ijayo. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kongamano hilo Iran itapata fursa kuhakikishia ulimwengu kuhusu mipango yake ya nyuklia kuwa ni ya amani.