Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto katika eneo la Lichinga Msumbiji wanasoma kuhusu hatari za kipindupindu
© UNICEF/Ricardo Franco

WHO: Kipindupindu chazidi kusambaa duniani

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO hii leo limetoa muhtasari wa ugonjwa wa kipindupindu ulimwenguni ambao mpaka sasa umetajwa kuenea katika mataifa 24 katika kanda tano za shirika hilo huku Afrika ikirekodi idadi kubwa ya wagonjwa. 

Kundi la watu wenye ulemavu ambao wanashiriki Jukwaa la WEIF 2024
UN News/Abdelmonem Makki

Azimio la 5 la Manama lapitishwa, watu wenye ulemavu waonesha ubingwa wao kwenye ugunduzi

Azimio la 5 la Manama limepitishwa hii leo huko Manama, mji mkuu wa Bahrain na washiriki wa Jukwaa la Kimataifa la Uwekezaji kwa Wajasiriamali likiwa na wito wa pamoja na mambo mengine  likisihi jamii ya kimataifa na wadau wote katika sekta ya umma na binafsi kutumia nguvu ya ujasiriamali na uwekezaji katika nyanja zote za kiuchumi na kijamii kama kitovu cha kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kupatia kipaumbele makundi maalum wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake, vijana na familia zinazohaha kutumia uwezo wa kuzalisha ili kujikimu kimaisha.

Fatou Haidara, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO na Mkurugenzi Msimamizi wa Idara ya Ubia wa Kimataifa UNIDO (kulia) akiwa na Abdulla bin Adel Fakhro,, Waziri wa Viwanda waBahrain kandoni mwa ufunguzi wa WEIF 2024, Manama, Bahrain
UNIDO-ITPO

WEIF2024 yaanza Bahrain ikilenga kuchochea ugunduzi na ujasiriamali

Jukwaa la tano la kimataifa la uwekezaji kwa ujasiriamali, WEIF2024 linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa limeanza leo huko Manama, Bahrain likiwa na wawakilishi wa serikali, mashirika ya kiraia, wawekezaji, wasomi na wabunifu na wakitoka pembe zote za dunia kwa lengo la kusaka mbinu za kuchochea ubunifu na ugunduzi ili hatimaye kusaidia kusongesha malengo ya maendeleo endelevu.