Mkutano wa dunia kuhusu afya wakubaliana kuhusu marekebisho ya Kanuni za Afya za Kimataifa
Katika hatua ya kihistoria, Mkutano wa 77 wa Dunia kuhusu Afya (WHA77), ambao ni mkutano wa kila mwaka wa nchi wanachama 194 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, leo umekubali fungu la marekebisho muhimu ya Kanuni za Afya za Kimataifa (2005) (IHR) na kutoa ahadi madhubuti za kukamilisha ndani yam waka mmoja mazungumzo kuhusu makubaliano juu ya janga la afya la kimataifa ndani ya mwaka, ikiwezekana mapema iwezekavyo.