Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kibao cha kupiga marufuku uvutaji wa sigara kwenye eneo la bustani ya  mboga katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New  York, Marekani.
UN News/Yasmina Guerda

Matumizi ya tumbaku mwaka 2023 yalipungua: WHO

2023 ulikuwa mwaka wa changamoto nyingi, halikadhalika mafanikio mengi, amesema Dkt. Tedros Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO wakati akiwasilisha ripoti yam waka jana ya shirika hilo mbele ya wajumbe wa mkutano wa 77 wa Baraza la shirika hilo huko Geneva, Uswisi. Miongoni mwa mafanikio hayo ni kupungua kwa matumizi ya tumbaku katika nchi 150, na kwamba kwa sasa kuna watumia tumbaku wachache milioni 19 ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita.

Wajumbe wa mkutano wa watoto na vijana kutoka nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, SIDS akiwemo Adelaide Nafoi kutoka Samoa (wa pili kutoka kushoto) baada ya kukamilisha kipengele chao cha “ukuta wa ahadi”.
UN News/ Matthew Wells

Huko Antigua, vijana wa visiwani wajenga “ukuta wa ahadi kukabili janga la tabianchi”

Yaweza kuwa ni ukuta uliojengwa kwa maboksi yaliyorejelezwa, lakini pindi viongozi wa dunia watakapokutana kuanzia kesho Jumatatu kwa ajili ya mkutano wa Nne wa Kimataifa wa nchi za visiwa vidogo zinazoendelea, SIDS4, moja ya makaribisho watakayolakiwa nayo ni ukuta wa ahadi kutoka kwa vijana ukielezea matumaini yao kwa dunia bora kwa kila mtu ili viongozi hao wachukue hatua kukabili madhara ya tabianchi.