Israel yakumbushwa kutekeleza wajibu wake wakulinda watu wenye ulemavu
Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Watu Wenye Ulemavu hii leo imeeleza kuwa watu wenye ulemavu walioko Gaza wapo kwenye hali ngumu na watakuwa wa kwanza kuuawa kutokana na fursa chache za kuwawezesha kukimbia maeneo ambayo Israel inatangaza wanatakiwa kuondoka kabla haijafanya mashamulizi.